WACHEZA KAMARI WACHAPWA BAKORA MSIKITINI
07:00 |
Watu nane walichapwa bakora mbele ya watu 1,000 ndani ya msikiti nchini Indonesia baada ya kuvunja sheria ya Kiislamu kwa kucheza kamari.
Mwendesha mashtaka wa nchi, kwenye jimbo la Aceh, kaskazini-magharibi mwa Sumatra, alisoma adhabu hiyo mbele ya mtu aliyejifichwa uso akiwa amevaa nguo ndefu ya hudhurungi.
Akitumia fimbo nyembamba ya mti wa mpingo, aliwachapa kwenye makalio watu hao fimbo tano kila mmoja.
Watu hao walichapwa bakora tano kila mmoja kwa fimbo ya mti wa mpingo katika eneo la msikiti wa jimbo la Aceh, Indonesia.
Msikiti ulijawa na watu wakati wa adhabu hiyo iliyofuatiwa na ibada ya Ijumaa asubuhi.
Adhabu hiyo ya fimbo ilifuatia baada ya kukamatwa watu tisa kwa kucheza kamari mwezi Julai. Polisi walikamata kisasi cha pauni 80 (208,000) kutoka kwa watu hao.
Adhabu hiyo ilifanywa na mtu aliyekuwa amevaa nguo ndefu ya hudhurungi baada ya mashtaka kusomwa na mwendesha mashtaka wa nchi.
Mmoja wao hakuweza kuchapwa kwa sababu ya afya yake ila atakabiliana na adhabu hiyo atakapopona, alisema mwendesha mashtaka wa nchi Nurhalma ambaye anatumia jina moja tu.
Related Posts:
NOMAA::MWANAMKE ALIYETEMBEA NA WANAUME ELFU 10 AJITOKEZA Mwanamke mmoja ameamua kujitokeza hadharani na kusema kuwa katika maisha yake tayari amekwishatembea na wanaume elfu 10 asilimia 90 wakiwa … Read More
INASIKITISHA::MSICHANA MIAKA 18 ASHIRIKI NGONO NA WANAUME 24 HADHARANI ILI ASHINDE KINYWAJI CHA BURE,:CHEKI HAPA Kiu ya kushinda zawadi yenye jina lililomsafirisha kimawazo imemponza msichana mmoja Muingereza baada ya kuamua kutoa utu wake na kukubali kushir… Read More
R,KELLY AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU JINSIA MBILI ZA MTOTO WAKE R. Kelly’s transgender son, Jay Kelly made headlines when he came out as a transgender boy. Jay, who lives with his mother Drea Kelly, requested… Read More
MAAJABU::MTOTO AZALIWA NA MIGUU MITATU, ATARAJIWA KUFANYIWA UPASUAJI Mtoto mdogo ambaye amezaliwa na miguu mitatu amesafirishwa kwenda nchini Marekani kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji kuondoa miguu miwili Ana Paula m… Read More
MAMA AMCHOMA KISU NA KUMUUA MWALIMU MBELE YA WANAFUNZI WAKE Mwanamke mmoja ameripotiwa kumchoma kisu na kumuua mwalimu wa kike wa shule ya msingi mbele ya wanafunzi wake katika mji wa Albi ulio kusini mwa … Read More