HABARI MPYA

Monday, 7 September 2026

KWA NINI WAGANGA WANAWEZA KUWASAIDIA WATU KUWA MATAJIRI WAKATI WAO NI MASIKINI?



Kuna watu ambao wanapata mafanikio makubwa kwa kutumia uchawi. Ila mafanikio yale hayaletwi na uchawi bali imani ya mtu husika.

Tutajadili kwa nini waganga wanaweza kuwapatia watu wengine dawa au mbinu za kuwa matajiri wakati wao ni masikini. Na pia tutaangalia jinsi ambavyo unaweza kutumia mbinu hizi wanazotumia waganga bila ya wewe kuwa mchawi na ukafikia mafanikio makubwa.


Kila mmoja wetu anaelewa kwamba kuna watu wanakwenda kwa waganga na wanasaidiwa kupata utajiri. Japokuwa utajiri huu haudumu, lakini angalau wanaupata kwa kiwango fulani.


 

 Wakati waganga hawa wanawasaidia watu kuweza kujenga magorofa, wao bado wanakaa kwenye vibanda vya nyasi.


Sasa kwa nini wao wasingetumia uchawi wao na kuwa matajiri zaidi ya hao wateja wao? Ina maana wao hawapendi utajiri huo?


Mbinu za waganga kuwasaidia watu kupata utajiri.

Watu wanaokwenda kwa waganga ili kupata utajiri au mafanikio yoyote hupewa masharti ambayo ni magumu kwa kiasi fulani. 


Na watu hawa huambiwa wakivunja masharti hayo tu utajiri wao unaisha mara moja. Ni masharti haya ambayo humjengea mtu nidhamu kubwa sana na kumfanya aweze kufanya kazi kwa juhudi kubwa kuliko wengine ambao wanafanya anachofanya. 


Kwa mfano mganga anamwambia mtu kila siku aamke asubuhi na mapema sana na apasue nazi barabarani ndio aende kwenye biashara zake. 


Kupasua nazi hakuna uhusiano wowote na mafanikio yake ila kuamka asubuhi na mapema kila siku ina msaada mkubwa kwenye mafanikio yake.


Hivyo mtu huyu atafuata masharti haya kila siku na hata kama kuna siku hajisikii itambidi afanye tu kwa sababu ameshaaminishwa akiacha atafilisika.


Sasa wewe ambaye huna sharti la aina hii siku ukiwa hujisikii vizuri unalala, siku nyingine unachelewa na hivyo kushindwa kufikia mafanikio makubwa. 


Masharti mengine kama kutokufanya starehe, kutokunywa pombe, kuvaa nguo moja na mengine mengi yanapelekea mtu kupunguza matumizi na kupata muda mwingi wa kufikiria kazi au biashara yake.


Masharti mengine yanayotolewa na waganga ni kumfanya mtu aweze kuondoka kwenye woga wake(comfort zone). Kila mmoja wetu kuna vitu fulani anaogopa kufanya, lakini vitu hivi ndio vinaweza kumletea mafanikio.


 Ili kukuondolea woga huu mganga anamfanya mtu afanye jambo kubwa sana ambalo litamuondolea woga kabisa.


 Kwa mfano mtu anaambiwa aue, kwa kuona kwamba ameweza kuua mtu, inamfanya mtu asizuiwe na kitu chochote.


Kikubwa ambacho mganga anamsaidia mtu ni kumjengea utaratibu ambao lazima kila siku ataufuata na pia kumjengea nidhamu binafsi na hivyo kuweza kufanya jambo hata kama hajisikii kufanya. Na hili ndio hitaji kubwa la kuweza kufikia mafanikio.


Kwa nini waganga hawawezi kutumia mbinu hii wenyewe.?

Kwa sababu wanajua inavyofanya kazi na pia hawana mtu wa kuwajengea imani hiyo kubwa kwao wenyewe.


Kwa nini watu baadaye hufilisika?

Wengi hufilisika baadae kwa sababu wanapopata mafanikio wanasahau kutumia yale masharti waliyopewa na pia imani yao inakuwa imewekwa kwenye vitu fulani(mfano hirizi) badala ya kuwa kwao wenyewe.


Ufanyeje ili uweze kutumia mbinu hii kufikia mafanikio.

Cha kwanza kabisa lazima ujijengee nidhamu binafsi. Jiwekee masharti yako ambayo utayafuata kila siku na hakikisha unayafuata.


Kwa mfano weka utaratibu kwamba kila siku utakuwa unaamka saa kumi asubuhi, kuipanga siku yako na kisha kujisomea kidogo. 


Baada ya hapo unawahi kwenye eneo lako la kazi au biashara na kuanza kazi zako mapema. Pia unaweza kujiwekea utaratibu kwamba kila mteja au mtu yeyote unayekutana naye kwenye siku husika atajisikia vizuri kukutana na wewe.


Fuata masharti haya kila siku na utaona mabadiliko makubwa kwenye maisha yako na shughuli zako.

Kwa hiyo mpaka sasa una mbinu mbili za uhakika za kufikia mafanikio;

1. Una uwezo mkubwa uko ndani yako, ila unatakiwa kuwa na imani kubwa sana kwamba unaweza kupata kile unachotaka.

2. Lazima uwe na nidhamu binafsi, uwe na masharti(rituals) na uwe na utaratibu wa kufanya kila siku (routine). Vitu hivi jiwekee mwenyewe na vifuate kila siku kwenye maisha yako.

Ukiweza kufanya mambo hayo mawili ni lazima utafikia mafanikio makubwa.

Nakutakia kila la kheri katika kufikia mafanikio. Kumbuka unaweza kufanikiwa kwa kiwango kikubwa sana bila ya kutumia uchawi au kwenda kwa mganga.Uchawi kamili upo kwenye kichwa chako. Anza kuutumia sasa.

credit- Makirita Amani-(Amka mtanzania)

IF YOU SEE THIS, YOUR RELATIONSHIP IS FALLING APART


Hello and welcome to this page.  We have all seen the signs a relationship is falling apart. How often have you gone to a restaurant and watched a couple not speak a word to one another? They stay married for the sake of being married and mechanically go through the daily motions of life. 

These couples have nothing in common and most likely have not embraced each other for years. No affection. No emotion. No warmth between them.

They may have been in love at one time, or maybe they weren’t. The fact is that they are no longer in mutual love. These couples may have grown tired of each other or taken two different paths in life. Many relationships fall flat in what is known as the “convenient” stage of marriage.

Why do relationships fall apart?

Relationships can fall apart due to several reasons. Usually, it is not just one reason a relationship would fall apart. It is primarily a combination of several factors. 

  1. Loss of trust
  2. Lack of communication
  3. Lack of respect
  4. Lack of intimacy
  5. Different priorities
  6. Lack of effort

Here are 10 signs your relationship is falling apart

How to save your relationship starts with acknowledging the signs your relationship is failing.


1. Lack of intimacy

Lack of sex, intimacy, or touch is one of the first signs of your relationship falling apart. Sex is the glue that cements your relationship as a couple. It’s special and sacred to just the two of you. It’s a powerful act of togetherness that keeps you centered and connected.

Without sex and affection, the two of you have become good pals. A marriage falling apart will exhibit the signs your relationship is falling apart.

2. Poor communication (or none at all)

How to know if your relationship is falling apart? When there is an evident lack of communication.

Lack of daily communication with your partner is one of the signs your relationship is falling apart. When relationships start to crumble, silence is generally one of the first indicators. When loving text messages, emails, and phone calls become scarce or non-existent, it could be time for a relationship check-up.

If you ask whether “my relationship is falling apart?” then bridging the communication gap with your partner is pivotal in understanding how to save a relationship.

3. PDA is non-existent

If your public displays of affection have become public displays of separation, you may have cause for concern. Touch is driven by love. When you are in love, you want to touch your partner.

When sweet kisses, hand holding, and walking arm-in-arm have been replaced by crossed arms and a measurable distance between you, those are obvious signs your relationship is falling apart.

4. Terms of endearment are rarely used

You will witness an elevated formality with your partner when you feel like your relationship is falling apart. When “Sweetheart,” “Honey,” and “Lover” have been replaced with “Angela,” “Jack,” and “Stacey,” you might want to listen up.

The way your spouse addresses you exudes signs your marriage is falling apart. Love elicits loving terms of endearment. Your boss should call you by name; your partner should not.

What are the reasons that marriages fall apart? Watch this video to know more.

5. No more common interests

Doing activities as a couple strengthens your bond. Mutual interests keep you connected as a couple. When you explore life as a tag team, you look forward to your time together. It’s like being married to your best friend, with the bonus of sex. 

When your relationship is falling apart, the interests you once enjoyed together might have become strictly solo adventures. 

What to do when your relationship falls apart from a lack of common interests?

Well, you may need to restructure your interests to merge back together as a couple. How to fix a relationship that’s falling apart sometimes necessitates putting the interests of your partner before yours.

With a fragment of love and attraction still felt by both of you, your relationship may require a bit of polishing to reboot and get back on track.

6. You don’t spend time together

All date nights and quality time together are now almost non-existent. You both have stopped spending any time together. Even if you live in the same house or room, there are barely any conversations.

7. You keep secrets

How much do you both know about each other’s lives at this point? If the answer to that is “not much,” chances are that, unfortunately, your relationship is falling apart. 

If either of you are doing things you do not want the other to find out or are just secretive because you do not want them to be a part of your life, it could be one of the signs.

8. You lose your temper easily

If everything your partner does has started to irk you, it could be one of the signs that your relationship is falling apart. The little endearing things about them have become the most annoying bits of their personality. 

9. You’ve run out of compromises

Compromises are a part of relationships. Now and then, one person compromises to make sure the relationship remains healthy and smooth. However, if one partner starts to feel like they are the only one who compromises for the sake of the relationship or feels like they have run out of them, it could be one of the signs your relationship is falling apart.

10. You lose your sense of self

If the relationship encroaches upon your sense of self – your self-respect, individuality, or self-worth, it could be one of the signs that your relationship is falling apart. If you are not happy and satisfied as an individual, it gets tough to be happy in a relationship.

Once you determine if an aspect of attraction is left in your relationship, how do you go about pulling your relationship out of the fix-it stage? Easy! You put in the effort.

USHIRIKIANO PSSSF NA TBN KUCHOCHEA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII

 




Na Mwandishi wetu

Dar es Salaam

Katika kile kinachoelezwa kuwa ni hatua madhubuti ya kupanua wigo wa utoaji wa elimu kwa umma, timu ya maofisa wa juu kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) imefanya ziara rasmi katika makao makuu ya muda ya Tanzania Bloggers Network (TBN) yaliyoipo Dar es salaam, Kijitonyama na kufanya mazungumzo ya kimkakati na viongozi wakuu wa mtandao huo.

Mazungumzo hayo yaliyolenga kujenga ushirikiano wa manufaa ya pande zote mbili  yamejikita katika kuimarisha uhusiano wa kisekta kwenye masuala ya habari, uelimishaji wa umma, na usambazaji wa maarifa sahihi kuhusu mifumo ya pensheni na uwekezaji nchini.

Akizungumza wakati wa mkutano huo, Mwenyekiti wa TBN, Beda Msimbe, alieleza utayari wa mtandao huo kusimama kidete kama chombo cha kutoa elimu na kusambaza maarifa sahihi kwa umma na katika nyanja za kidijitali (space). Hata hivyo, alisisitiza kuwa ili kufikia malengo hayo kwa ufanisi zaidi, ni muhimu wanachama wa TBN wenyewe wakapatiwa kwanza mafunzo ya kina na ya kutosha kuhusu shughuli na uendeshaji wa mfuko huo.

Ushirikiano huo unatazamiwa kufungua ukurasa mpya katika matumizi ya vyombo vya habari vya mtandaoni kufikisha elimu ya hifadhi ya jamii kwa wananchi wengi zaidi nchini.

Kwa upande wake, Mkuu wa msafara huo kutoka PSSSF, Abdul Njaidi, alieleza kuwa ziara hiyo inalenga kujenga uhusiano wa karibu na wadau wa sekta ya habari pamoja na kutoa elimu kwa jamii. Aliwahakikishia viongozi wa TBN kuwa maombi na hoja zote zilizowasilishwa zitafanyiwa kazi, akisisitiza kuwa ushirikiano huo mpya unalenga kuhakikisha wananchi wanapata uelewa mpana na sahihi kuhusu masuala ya pensheni na uwekezaji unaofanywa na PSSSF.

Naye Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi, ambaye alishiriki katika mkutano huo, alieleza kuwa mtandao huo wenye historia kubwa unajivunia weledi na ufanisi mkubwa. 

Alisema TBN ipo kwa ajili ya kuhakikisha Tanzania inasomeka vyema katika medani za kidijitali ili kuchochea na kutanua zaidi gurudumu la maendeleo ya taifa.

Katibu wa TBN, Rahel Pallangyo, aliongeza kuwa mtandao huo upo tayari kutoa waandishi wake mahiri na kutumia majukwaa yake mbalimbali kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi na za kuaminika zitakazowezesha kufanikiwa kwa utekelezaji wa majukumu ya wananchi na wadau wa maendeleo.

Katika mkutano huo, ujumbe wa PSSSF ulioongozwa na Abdul Njaidi, ulijumuisha maofisa wengine akiwemo Regina Kumba, Grayson Mgunda, na Doreen Lyimo. 

Kwa upande wa TBN, viongozi waliohudhuria ni pamoja na Mwenyekiti Beda Msimbe, Katibu Rahel Pallangyo, mtaalamu wa mawasiliano, Cathbert Kajuna na Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi.

Friday, 4 September 2026

TCAA NA UMOJA WA ULAYA WATHIBITISHA DHAMIRA YA KUIMARISHA USIMAMIZI WA USALAMA WA USAFIRI WA ANGA

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari, amethibitisha dhamira ya Mamlaka hiyo ya kujenga Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya kiwango cha kimataifa barani Afrika, yenye matarajio ya kufikia viwango vinavyolingana na mamlaka za usafiri wa anga za Ulaya katika ubora wa udhibiti, umahiri wa kitaalamu, ufanisi wa kiutendaji na usimamizi wa usalama wa anga.

Alitoa kauli hiyo wakati wa kikao cha kuhitimisha ujumbe wa wataalamu wa msaada wa kujengeana uwezo kutoka Shirika la Usalama wa Anga la Umoja wa Ulaya (EASA), kilichofanyika tarehe 3 Septemba 2026 katika Makao Makuu ya TCAA jijini Dar es Salaam. Dkt. Bakari aliushukuru Umoja wa Ulaya kwa kuendelea kutoa msaada na kuonyesha imani katika maendeleo ya Tanzania. Pia alieleza juhudi zinazofanywa na TCAA kuimarisha mifumo yake ya usimamizi, ikiwemo uundaji na utekelezaji wa Mfumo wake wa ndani wa TCAA wa Huduma za Usafiri wa Anga (Civil Aviation Services Portal – CASP), ambao ulipewa pongezi na timu ya EASA.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Dkt. Jabiri K. Bakari akizungumza   wakati wa kikao cha kuhitimisha ujumbe wa timu wataalam kutoka  Shirika la Usalama wa Anga la Umoja wa Ulaya (EASA)


Timu ya EASA ilieleza kuridhishwa kwake na maendeleo na juhudi zilizooneshwa na TCAA wakati wa ziara hiyo ya siku tatu. Aidha, timu hiyo ilitambua maendeleo yaliyofikiwa na kuhimiza TCAA kuendeleza kasi katika kushughulikia masuala yote muhimu ya usimamizi wa usalama wa anga.

Kwa upande wake Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Ulaya alithibitisha dhamira ya EU ya kuendelea kuisaidia Tanzania kupitia msaada wa kitaalamu, mbinu za utekelezaji wa vitendo na kubadilishana ujuzi. Aidha, alieleza kuwa Umoja wa Ulaya umetenga Euro milioni 2 kwa ajili ya msaada unaohusiana na kuboresha zaidi Masuala ya usafiri wa anga nchini. 




Kiongozi wa Ujumbe wa EASA Bw. Jose Miguel Manso Angulo akizungumza wakati wa kikao hicho

Ujumbe wa EASA uliongozwa na Bw. Jose Miguel Manso Angulo akiambatana na Bw. Gustavo Juan Roman Barba na Bw. Antonio Portales Pelaez.

Ujumbe huo, uliopo nchini kwa siku tatu kuanzia tarehe 1 hadi 3 Septemba 2026, ulifuatilia maendeleo ya Nchi (State) katika utekelezaji wa hatua za marekebisho pamoja na kuimarisha usimamizi wa usalama wa Usafiri wa anga. Majadiliano yalihusu maeneo ya ki sheria, muundo wa taasisi, uchunguzi wa ajali ndege, utoaji wa leseni kwa eneo la rasilimali watu la Usafiri wa anga, ubora wa ndege kwa matumizi (airworthiness) na uendeshaji wa ndege, pamoja na kufanya vikao na waendeshaji wa mashirika ya ndege kuhusu hoja zilizobainishwa, Mipango ya Hatua za Marekebisho (Corrective Action Plans) na ufuatiliaji wa utekelezaji wake.

Ujumbe huo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za Tanzania za kuimarisha usimamizi wa usalama wa Usafiri wa anga na kuonesha maendeleo endelevu kuelekea kutimiza matakwa ya kuondolewa kwenye Orodha ya Usalama wa Anga ya Umoja wa Ulaya (European Union Air Safety List).

Thursday, 3 September 2026

UKIZITUMIA KAULI HIZI KUMFARIJI MTU ZITAZIDISHA HUZUNI KWA MUHUSIKA


Haya ni makosa ambayo tunayafanya bila kujua, kwasababu katika muda huo, tunakuwa hatuna njia ya kumfanya aliyeondokewa na mali au mtu ajisikie tuko pamoja naye katika machungu.

Na kwakuwa ni vigumu kwa muhusika kukueleza kwamba nataka kufanyiwa au kuambiwa kitu fulani ndio nitajisikia vizuri, inakubidi utumie ujuzi wako binafsi kutafuta njia ya kumfanya ajisikie vizuri.

Hapo sasa balaa ndio linaanza,kwani mara nyingi maneno tunayochagua kumwambia aliyepotelewa hayamfanyi ajisikie poa bali yanamfanya aanze kutafakari ulikuwa na maana gani.

Na hii inatokana na si wote wana uwezo wa kutafakari kauli zinazotolewa na watu wengine katika mtazamo chanya.

Hebu tuangalie maneno ambayo hupaswi kuyasema  kwa muhusika:

1."Shukuru (ameishi/umeishi nacho) miaka mingi"

Unapoongea kauli kama hii inampa picha mtu huyo, kwamba jambo hilo lilipaswa kutokea kwake,na hivyo hapaswi kuhuzunika.Yawezekana kuna ukweli ndani yake, lakini unapoongea mbele ya muhusika haitamfanya ajisikie vizuri.

2."Muda wake ulifika"

Hata kama umekosa la kuongea hii kauli sio kabisa,itamfanya akuone umefurahia tukio hilo.

3."Alikosea/Ulikosea sana ku.... "

Ikiwa tukio lilikuwa la ajali, hata kama liliempata alisababisha usiongee kauli kama hii kwa muhusika,itaonekana kana kwamba alifanya uzembe na alistahili kupatwa na hilo.

4."Kuna sababu ya kila kitu"

Hii  kauli kweli ina maana, unapofikiria kwa kina lakini si nzuri kuizungumza kwa mtu aliye kwenye majonzi.

5."Usihofu utampata mwengine tu"

Ikiwa mtu amepoteza mtoto, mume au mke, kauli ya kumwambia kwamba asihuzunike na kuwa atapata mwengine tu,itamfanya aone hukuwahi kuona umuhimu wa aliyeondokewa naye,na ulikuwa unaombea hilo litokee.

Mara nyingi maneno haya yanapotamkwa na muhusika yanakuwa na matumaini zaidi kuliko yanapotamkwa na mtu mwengine wa pembeni. 

Ni heri utumie maneno kama:

1."Pole sana kwa yaliyotokea" 

2."Natamani ningekuwa na maneno mazuri ya kukueleza ujisikie vizuri"

3."Niko pamoja nawe katika hili"

4."Niko pamoja nawe katika sala"

5."Tulimpenda wote"

6."Ukihitaji msaada, niko hapa kwa ajili yako"

TABIA YA KUWAFARIJI WENZETU WANAPOPATWA  NA MATATIZO, NI NZURI SANA NA ITAWAFANYA  WAJISIKIE VIZURI.

KWELI YAWEZEKANA UNA TAFSIRI YAKO MOYONI JUU YA TUKIO LILILOTOKEA,  LAKINI IWEKE MOYONI UKIONA HAITAMFARIJI MUHUSIKA.

WOTE TUNAWEZA KUWA TUMAINI KWA WENGINE PALE WANAPOPATWA NA  MATATIZO 
KWA KUTUMIA MANENO NA NJIA SAHIHI 


KUELEZEA HISIA ZETU PIA.

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA