HABARI MPYA

Tuesday, 3 February 2026

KAMA KWELI UNAHITAJI MWENZI WA MAISHA: HII INAKUHUSU



 
Ni njia gani za kumpata mwenzi wa maisha yako? Inawezekana unakabili mtihani mzito, hujui ni yupi wa nafsi yako. Bila shaka unamtaka yule wako wa kufa na kuzikana.

Mada hii inakuja na suluhisho mahsusi kwako, kumjua mapema anayekufaa, anayeweza kudumu nawe maishani. Zingatia kwamba mwenzi sahihi wa maisha yako ni hatua muhimu kuelekea kwenye mafanikio.

KWANZA TAMBUA HILI

Uhusiano wa kimapenzi ni suala binafsi. Kwanza kabisa ni sanaa inayokutaka uangalie mahitaji yako mwenyewe. Je, unahitaji nini kwa mtu ambaye ungependa awe mwenzi wa maisha yako?

Yale unayotaka kutoka kwa mtu ambaye unapenda awe mwenzi wa maisha yako, unapaswa kuyapa kipaumbele. Hata siku moja, usithubutu matamanio ya mwili na moyo yakupe mwongozo wa kumwona umpendaye.

NANI MWENZI WA MAISHA?

Ni swali ambalo unapaswa kujiuliza. Kwa uwazi kabisa, unatakiwa kuzingatia kuwa mwenzi wa maisha ni yule ambaye utachangia naye mambo mengi kwa uaminifu na maelewano makubwa.

Mwenzi wa maisha si mtu unayeweza kuwa naye kwa mantiki ya kupeana tulizo la ngono unapohitaji au kampani ya kwenda kuangalia ‘muvi’, muziki, ufukweni na kwingineko unapoona huhitaji kuwa peke yako.

Mwenzi wa maisha ni yule atakayefanya ujione umekamilika, bila kujali ‘ubize’ wala ukapa ambao pengine unao ndani ya jamii inayokuzunguka. 

Kingine cha kuzingatia ni kwamba, mwenzi wa maisha yako ni yule ambaye anakukubali na kukupenda kama ulivyo, bila kuwepo kwa nyongeza ambazo zitatokana na kukubadilisha kutoka yule wa zamani.

Kupata mwenzi wa maisha mwenye sifa kamili, ni sawa na kupatia herufi ya mwisho kwenye mchezo wa kubahatisha. Kwa maana hiyo, baada ya kumpata, kila kitu kinakuwa kimekamilika maishani mwako.

NANI MWENZI WA MAISHA YAKO?

Pointi ya msingi kuzingatia ni kwamba unahitaji kuwa na yule anayekubalika ndani ya nafsi yako. Hivyo basi, fikiria kwa yale yanayoweza kukufanya uwe na furaha, pia yanayoweza kukupa huzuni.

Zingatia mapitio yako ya nyuma kuona ni kwa namna gani yamekutengeneza mpaka kufika ulivyo sasa. Jiulize pia kuhusu ndoto na malengo yako siku za usoni.

Ikiwa tu utaweza kutambua mahitaji na matarajio yako ya kimaisha, bila shaka utaweza kutambua ni mtu gani anayefaa katika kukusaidia kutimiza kila kilichomo ndani ya malengo yako.

JENGA IMANI

Kutafuta mwenzi wa maisha siyo suala la kuangalia mtu wa kwenda naye klabu kujirusha usiku. Vile vile ni muhimu kutambua kwamba inaweza kukuchukua muda kupata mtu wa kukidhi vigezo vyako.


Pamoja na ukweli huo, bado unatakiwa uwe na imani kwamba itafika wakati utasahau habari za kutafuta mwenzi na utakuwa mwenye furaha, ukijipongeza kwa kumpata anayekufaa.

Mapenzi ni mchezo lakini ni rahisi kuucheza ukitambua kanuni zake. Hii ina maana kuwa unapokuwa kwenye kipengele hiki, unakuwa na jukumu moja zito la kuhakikisha unampata yule mwenye uwezo wa kukonga moyo. Mwenye sura ya kutimiza malengo yako.

Hata hivyo, muhimu kwako ni kuwa mtulivu na kuacha macho yafanye kazi ya kuangaza kwa utaratibu, halafu akili ifanye kazi ya kutathmini kiwango cha huyo atakayeonwa.

Kitu kingine ambacho unatakiwa kuheshimu ni kuwa, wawili wanaopendana, kila mmoja kwa nafasi yake ni nusu ya kitu kizima kinachoitwa ndoa au wapenzi, hivyo wanapounganishwa ndiyo kinapatikana kitu kizima.

Ukiamini kuwa wewe ni nusu na utakamilika baada ya kukutana na mwenzi wako, unachotakiwa kufanya ni kujenga imani kwamba mwenzi wako yupo sehemu kwa ajili yako, hivyo endelea kumtafuta na siku moja utamuweka mikononi mwako. 

Friday, 16 January 2026

MAMBO MUHIMU KWA VIJANA WENZANGU.!

MUHIMU KWA VIJANA WENZANGU.!
Na Kdmula

Wengi itakuwa bado miaka miwili, mitatu au minne kabla ya kutimiza miaka 30. 

Natambua kuwa kuna waliokwisha fikisha na kuna uwezekano kuna walio nyuma kidogo.
Kama katika umri tulionao sasa kuna mtu anakuambia wewe bado ni mdogo/mtoto, basi huyo mtu hakupendi na anakulemaza kiakili. Kua! Acha utoto! Mambo yafuatayo kwa vigezo vya kibinadamu mwenye akili timamu, mtu mwerevu lazima uwe ushayatimiza.

1) Kuweka misingi ya kifamilia:
Katika umri huo unatakiwa uwe umeoa, umechumbia au uko katika uhusiano wenye kueleweka unaelekea kwenye kujenga familia. Kama katika umri huu bado unabadilisha wanawake na kudandia vicheche, basi sahau kuwa na familia imara. Mambo yafuatayo yatakuwa yanakunyemelea;
– Kuoa/kuolewa msichana/mvulana mdogo sana ambaye atakuona unamzeesha
– Kuoa /kuolewa chapchap bila kuwaza
-Kuokoteza magonjwa ya hatari
– Kunogewa na usela na kusahau kuoa/kuolewa
2)Kujitegemea kiuchumi:
Hapa simaanishi kufanya kazi na kupata mshahara pekee, la hasha! Hapa nalenga wale watoto wa mama ambao pamoja na kuwa wana kazi na mishahara, bado wanalalama mishahara haitoshi na kukimbilia kuomba hela nyumbani wanapoishiwa mara kwa mara. Wale ambao bado wanakaa nyumbani hii inawahusu pia. Pia wale wanaotumia 100% ya mishahara kununua vitu vinavyoisha (consumption) wakingoja wapate hela nyingi au wazazi, ndugu na jamaa wawasaidie kwenye uwekezaji. Africa tunachelewa sana kwenye hii sector.
3) Kuwa na kitega uchumi:
Kama unadhani mshahara wako wa milioni kadhaa ni mwingi sana, ngoja augue mtu wa karibu au wewe mwenyewe halafu daktari akuambie mgonjwa wako/wewe ana/unatakiwa ape/upelekwe nje ya nchi kwa matibabu zaidi wakati huna bima ya afya inayolipia hilo ndo utajijua kama mshahara wako heshima yake inaishia samaki samaki au inavuka border. Kitega uchumi si lazima uwe na mkampuni mkubwa, la hasha! Ila uwe na kitu cha kueleweka na chenye malengo ya kukua kuwa kitu cha maana. Kwa wale wagumu kuelewa, UNATAKIWA UWE NA PATO LA PEMBENI NJE YA MSHAHARA.
4) Makazi:
Uwe hata na kiwanja hapo Bunju Arif! Huezi kunywa bia kila weekend halafu wenzio wakiongelea issues za nyumba/viwanja/mashamba yao unakimbilia kubadilisha mada (Eti Huyu LVG wamuondoe kabisa anaharibu timu). Kumbe unazuga kupotezea story za viwanja/nyumba.
5)Uwe na professional qualification
: ACCA,CPA,CFA,CSIA,CPB, LAW SCHOOL ETC wale wa procurement wana ya kwao n.k. Ikifika huu umri kama CPA imekataa, tafuta hata mitihani za marketing upige, CPA sio issue zako. Lazima uwe na defined career (Kama hukubahatika kwenda kidato kingi, uwe na namna ya halali na ya kudumu ya kukupatia kipato). Umri huu kama huna utaalam katika fani yako, jiandae kuwa frustrated ofisini. Madogo wanasoma jamaa angu! Halafu wako tayari kupewa salary ndogo wapige kazi kuliko wewe.. So take care!
6) Uwe ushaamua ka hicho kitambi unakiondoa au unakilea:
Hapa sichekeshi! Kitambi kina madhara mengi. Suruali haikai vizuri, UTAPIGIWA, Kisukari, pressure n.k. Ukikinyamazia muda huu jua kitakuwa kishakomaa na majukumu yatakuwa mlima. Ukikiachia kijiamulie, kitakuganda kama “roba ya mbao” till death does you apart! Kama unakipenda endelea nacho, kama hukipendi uwe ushaweka program ya kukiondoa.
7)Uwezo wa kusaidia wanaokutegemea:
Kama we ni wa kishua, hapa hapakuhusu. Wewe ambaye si wa kishua, wazazi walikuwa na mategemeo flani walipokuwa wanakusomesha. Kama umefika miaka 30 hujaanza kuyatimiza mategemeo yao bila sababu ya msingi, jua watakuwa washakata tamaa na wewe.
8) Uwe na busara.
Kuwa mtu wa kufikiri kabla ya kutenda. Tengeneza haiba nzuri na ya kuheshimika kwa wanaokuzunguka. Kama huna busara hadi umri huu basi we sahau suala la busara ukiwa hai.. Labda utakutana nayo akhera.!
9) Savings:
Hapa nimeweka kizungu kuonyesha msisitizo. Kila mtu ana kipato chake. Ila formula ni kwamba angalau uwe ushahifadhi fedha sawa na mishahara yako ya mwaka na nusu gross of Tax kwa kipindi hicho. Kwa wale wagumu kuelewa namaanisha Ukiacha kazi au kusimamishwa kazi, uwe na uwezo wa kukaa mwaka na nusu bila kuingiza kitu chochote lakini uendelee kuishi maisha yale yale.
10) Umjue Mungu:
Nimeliweka hili mwisho si kwamba ni la mwisho kwa umuhimu, La hasha! Ni ili ulikumbuke zaidi. Mjue Mungu, mpende na umuogope. Nenda ibadani, soma neno lake na umuombe. Uwe na desturi ya kusali nyumbani kwako angalau kila unapoamka na wakati wa kulala. Kama humuogopi Mungu katika umri huu, basi wewe kwenda Mbinguni ni ngumu kuliko ngamia kupenya tundu la sindani (hata kama ni masikini).

Tuesday, 13 January 2026

MBINU SITA (6) SAHIHI ZA KUWEKA AKIBA ZAIDI NA KUWEKEZA VIZURI.


Kuna mambo mengi unayotaka kuyafanikisha katika kipindi hiki cha maisha yako. Bila ya kukanusha ,Ukweli ni kwamba baadhi ya ndoto zako zina gharimu fedha. Na ufunguo wa kuzifanikisha ndoto hizo ni kujifunza kusimamia fedha.

Pale unapokuwa umeshajifunza misingi ya kuhifadhi au kuweka akiba na kuwekeza fedha, bila shaka utaweza kuyafanikisha malengo yako.

Katika uchumi wa sasa wenye uhaba wa nishati na gharama za vyakula kuwa kubwa na kukua kwa kasi ya ukosefu wa ajira, kusimamia fedha kunaweza kukawa ni kazi ngumu sana ,lakini kwa hakika hakuna hata jambo moja lisilowezekana .Unawezaje kwenda na hali hii? Zifuatazo ni mbinu sita za kuweza kuweka akiba fedha nyingi zaidi na kuwekeza vizuri.

1. kuweka bajeti ni kipaumbele
Matumizi ya mara kwa mara na ya muda mmoja, kila aina ya matumizi , hata matumizi ya hiari. kama bajeti yako inahusisha vitu vyote hivyo, kuna uwezekano mkubwa sana wa wewe kutokuwa nje ya fedha, unaweza kusimamia fedha zako kwa kujiwekea bajeti tu. kwa njia hii unaweza kuwekea kipaumbele  matumizi yako  na kupanga fedha zako kwenye vitu vyenye umuhimu mkubwa sana kwenye maisha yako. ni muhimu kuweka na kutoa umakini kwenye vitu vidogo ambavyo vinaweza kuongezeka kwa kiasi kikubwa sana.

Kamwe usivipuuze vidogo vidogo au mambo madogo, hakika najua unataka vyote, lakini weka vipaumbele  kwenye vitu unavyovihitaji kwanza na vipi vya kusubiria kwa ajiri ya baadaye, Na kutumia kutokana na utaratibu huo.

2. Boresha rekodi ya matumizi.
Unahitaji kuangalia kwa makini na kwa karibu sana mahali fedha zako zinapokwenda  na wapi hasa unaweza  kukata pembe. magazeti ,Kunywa kahawa -vitu vyote vinahesabiwa,haijalishi unatumia kiasi kidogo cha pesa, vyote vinaongezeka na kuwa kiasi kikubwa sana, hivyo, unahitaji kufuatilia kila kitu. njia bora na iliyo nzuri ni kudumisha rekodi ya matumizi .jaribu kuandika na kuweka kumbukumbu juu ya vitu unavyotumia kwa zaidi ya mwezi. ukihusisha na kila manunuzi. kama utaweza kufanya hivyo kwa muda mrefu sana, utaweza kupata picha sahihi juu ya wapi hasa unatumia fedha zako na namna gani unaweza  kupunguza na kuweza kukata kabisa  gharama huko.

Katika Kuongeza na hili ,unaweza kugawanya matumizi yako katika makundi mawili; mara kwa mara na yasiyo ya mara kwa mara .hii itakusaidia kuwa na usimamizi wenye nguvu juu ya matumizi yako ya mwezi.

3. Futa madeni yote.
Kama upo kwenye madeni au unapambana kifedha, moja ya  njia rahisi sana kupambana na hali hii kutambaa kwenye magamba yako na kupuuzia nakala yako ya benki na mahitaji ya malipo. lakini hili ,kwa kutokuwa  na maana, inaenda kufanya vitu kuwa rahisi. badala yake ,kabili tatizo, jua unahitaji kushughulika na nini, Na ushakapokuwa  sahihi katika hili, utakuwa na ufahamu wa hatua inayofuata. ni muhimu  madeni yako yawe madogo vyovyote vile unavyoweza bila ya kuikabili biashara yako.

4.  Bima ni hatua ya kwanza.
Moja ya hatua ya msingi kwa ajiri yako na kwa familia yako hapo baadaye ni bima. kuna aina kadhaa za bima kama vile bima ya afya, bima ya ulemavu, bima ya umiliki wa nyumba.

5.  Anzisha lengo la kuweka akiba na weka akiba mara kwa mara.
Jitazame kwenye kioo na Kisha na useme hivi- Mwisho wa mwezi huu, utaweza kununua gari ya ndoto yako kutoka kwenye akiba yako, Moja ambayo umekuwa ukiisubiri mno kwa muda wote huo hii inakufanya hujisikiaje? msisimko? hakika! hii, kwa vyovyote vile ,haitoweza kuwa kweli mpaka pale utakapokuwa na busara na kuanza kuweka akiba fedha zako ili kufanikisha lengo lako. Jambo unalotakiwa kuliweka akilini mwako pale unapokuwa unaweka akiba fedha yako ,Ni kuweka umakini juu ya nini utaweza kufanya baada ya kuweza kufanikiwa kuweka  fedha nyingi ,Ni muhimu kujua hizo fedha unazoziwekea akiba utazitumia kwa ajiri ya nini, Utazifanyia nini? kuliko kufikiria tu kuweka fedha zako pembeni.

Ni muhimu kuwa na malengo ya kujiwekea akiba fedha zako. lakini watu wengi hawajui jinsi ya kuweka akiba fedha zao, kwa hiyo, Unataka kuweka akiba ya fedha mara kwa mara lakini haujui cha kufanya? Kama umeajiriwa;

Ingia akaunti ya kuweka akiba.
Weka maelekezo yenye msimamo, ili kila mwezi fedha yako iweze kupata kusafirishwa kwenye akaunti yako ya akiba moja kwa moja bila ya wewe kuwa na hofu kuhusu fedha yako. Na kamwe usisubiri mpaka mwisho wa mwezi kwa ajiri ya hili. Kwani kuna faida tatu za kufanya hivyo;

1.Fedha inapata kusafirishwa kwenye akaunti yako ya akiba mapema sana pale unapolipwa mshahara wako, kama umeajiriwa.

2. Kiasi ulichoweka akiba kitaongezeka ikiwa utapata ongezeko la mshahara na pia utapata Marejesho ya kiasi  ushindani juu ya akiba yako.

6. Tathimini uvumilivu wako wa hatari.
Hatari inafanya  kazi kubwa sana, Na ya muhimu kwenye kufanya maamuzi yote ya uwekezaji. kanuni ya shaba ni Inasema kwamba ,Kadri marejesho yanavyokuwa makubwa kutoka kwenye baadhi ya Sehemu za  uwekezaji, Ndiyo hatari inavyoweza kuhusika kwa ukubwa zaidi. Baadhi ya sababu muhimu zinaoweza kukusaidia kuamua uvumilivu wako wa hatari ni  kama vile Mapato, matumizi, malengo yako ya kifedha n.k.

kama unataka kufanya maamuzi yenye busara Au Yenye hekima kwenye uwekezaji, Unahitaji kutathimini uvumilivu wako wa hatari kabla ya kujiingiza kwenye kitu chochote kile.

Moja ya kitu kigumu sana kuhusu kusimamia na kuweka akiba fedha Ni hatua ya kwanza sana -kuanza. hii inaweza kuwa ni vigumu sana kutumia akiba yako kwa busara ili kuelekea kwenye malengo yako ya kifedha .
Mbinu zilizotajwa hapo juu zitakusaidia kwa kiasi kikubwa sana kuendeleza mpango wa ukweli wa kuweka akiba na kuwekeza. zaidi ya hapo, Zitakusaidia kuelewa mambo yanayohusiana na fedha kwa njia bora zaidi. Zifuate Mbinu hizo na hakuna lolote lile litakalokuzuia kuweza kufanikisha mafanikio ya kifedha. TUPO PAMOJA.
Geofrey Mwakatika

Mwakatikageofrey@gmail.com.  0767382324.

Saturday, 10 January 2026

NJIA ZA KUKABILIANA NA UCHOVU MWINGI

Image result for A TIRED BLACK PERSON
Uchovu unaotokana na kazi ni zaidi ya kuchoka kwa kawaida, na unazidi uchovu unaosababishwa na shughuli za kila siku. Dalili za uchovu huo ni kuchoka kupita kiasi kwa muda mrefu na vilevile kuhisi umekata tamaa na kukosa nguvu. Watu wanaokabili uchovu huo hawafurahii kufanya kazi zao, yaani, wanakosa hamu ya kufanya kazi na hivyo kuathiri ubora wa kazi. Utafiti pia unaonyesha kwamba kuchoka kupita kiasi husababisha matatizo ya kihisia na magonjwa.
Ni nini kinachosababisha uchovu mwingi?
Kwa kawaida kazi nyingi kupita kiasi ndicho chanzo kikuu. Kwa sababu ya matatizo ya kiuchumi, baadhi ya waajiri hutaka wafanyakazi wao wafanye kazi saa nyingi zaidi, na bila malipo ya kutosha. Maendeleo ya teknolojia hufanya iwe vigumu kwa watu fulani kutenganisha shughuli za kikazi na maisha ya binafsi. Nao wengine hupatwa na uchovu huo kwa sababu wanahofu kupoteza kazi zao, hawawezi kuzidhibiti, au wanahisi kwamba wanaonewa. Vilevile kutojua majukumu yao kazini au migogoro kati yao na wafanyakazi wenzao huchangia kuchoka kupita kiasi.
Uchovu mwingi pia unaweza kusababishwa na mtu mwenyewe. Ili wafikie malengo yao na kupata pesa nyingi, baadhi ya watu hufanya kazi zaidi ya moja. Watu hao wana majukumu mengi na wanakabili hatari ya kuchoka kupita kiasi.
Ikiwa unakabili tatizo la kuchoka kupita kiasi kazini, unawezaje kushinda tatizo hilo? Huenda ikaonekana vigumu kushinda tatizo hilo ikiwa kuna mambo yanayopita uwezo wako. Hata hivyo, chunguza hatua nne zifuatazo za kukabiliana na kuchoka kupita kiasi. Unaweza kupata suluhisho la tatizo lako.

1. CHUNGUZA MAMBO UNAYO YAPA KIPAUMBELE.

Ni nini muhimu zaidi kwako? Watu wengi wanasema kwamba uhusiano na familia zao na afya njema ndiyo mambo muhimu zaidi. Hivyo, ukichoka kupita kiasi familia yako itaathirika na afya yako itazorota.
Ukizingatia mambo muhimu, itakuwa rahisi kwako kufanya maamuzi magumu na kukataa majukumu fulani. Kwa mfano, unaweza kugundua kwamba kazi yako inakusababishia uchovu unaopita kiasi. Hata hivyo, huenda ukasema, ‘Siwezi kubadili kazi au kupunguza muda ninaofanya kazi; ninahitaji pesa!’ Ni kweli, kila mtu anahitaji pesa, lakini kazi yako inaathirije mambo unayothamini zaidi?
Uwe mwangalifu ili usitangulize mambo ambayo wengine wanaona kuwa muhimu. Huenda mambo ambayo ni muhimu kwa mwajiri wako yakatofautiana na mambo yaliyo muhimu kwako. Wengine wanaweza kutanguliza kazi kuliko mambo mengine maishani, lakini haimaanishi unapaswa kufanya hivyo.

2. RAHISISHA MAISHA YAKO.
Ili upunguze mkazo na upate muda wa kutimiza mambo unayothamini zaidi, huenda ukahitaji kufanya kazi kwa saa chache, kumwomba mwajiri wako akupunguzie majukumu, au ukahitaji kubadili kazi. Vyovyote vile, inaelekea utahitaji kupunguza matumizi ya fedha na kubadili mtindo wako wa maisha. Inawezekana kufanya marekebisho hayo, na huenda isiwe vigumu kama unavyowazia.
Katika nchi nyingi, wafanyabiashara wanashawishi watu wanunue bidhaa, na wengi wanafikiri kwamba furaha inatokana na kupata utajiri. Hata hivyo, si kweli. Maisha rahisi yanaweza kukuletea uhuru mwingi na kufanya uridhike. Ili ufanikiwe kufanya mabadiliko hayo, unahitaji kupunguza matumizi yako na kuweka akiba ya pesa. Jitahidi kupunguza au kuepuka madeni. Zungumza na familia yako kuhusu umuhimu wa mabadiliko hayo na uwaombe wakuunge mkono.

3. JIFUNZE KUFANYA  KAZI KWA KIASI.

Ikiwa una kazi nyingi kupita kiasi au tatizo lenye kudumu kazini, zungumza na mwajiri wako. Ikiwezekana, toa mapendekezo yanayofaa hali yako na pia mwajiri wako. Mhakikishie mwajiri wako kwamba unapenda kazi, na ufafanue yale ambayo uko tayari kufanya; lakini utaje waziwazi na kwa uthabiti mambo ambayo huwezi kufanya.
Mwanamume anayetazama saa yake
Uwe mwenye busara na uone mambo kihalisi. Ikiwa unataka kufanya kazi kwa saa chache, huenda mwajiri wako akapunguza mshahara wako. Fikiria pia uwezekano wa kufutwa kazi, na uwe tayari kukabiliana na hali hiyo. Si lazima uache kazi ili utafute kazi nyingine, ni rahisi kupata kazi nyingine ukiwa bado kazini.
Hata kama mwajiri wako atakubali ufanye kazi kidogo ujue kwamba huenda baadaye akasisitiza ufanye kazi zaidi. Ni nini kitakachokusaidia kudumisha msimamo wako? Jitahidi kudumisha makubaliano yenu ya awali. Kufanya hivyo kutakupa uhuru wa kumwomba mwajiri aendelee kufuata makubaliano hayo.

4. UWE NA MUDA WA KUPUMZIKA.

Hata ukifaulu kupunguza kazi, huenda bado utapatwa na mkazo, utashughulika na watu wagumu, au hali zisizopendeza. Uwe na muda wa kupumzika vya kutosha na uwe na burudani kwa kiasi. Kumbuka kwamba si lazima utumie pesa nyingi ili ufurahie burudani pamoja na familia yako.
Mbali na kazi, uwe na mambo unayofurahia kufanya na pia uwe na marafiki, na uepuke kufikiria kazi tu kila wakati. Kwa nini? Kitabu Your Money or Your Life kinasema hivi: “Utu wako ni muhimu kuliko kazi unayofanya ili kupata pesa.” Ikiwa unafikiri utambulisho wako au heshima yako inategemea kazi yako, huenda ukashindwa kuweka mpaka kati ya kazi na shughuli zako mwenyewe.

Thursday, 8 January 2026

TRUST ME,WE NEED OTHER PEOPLE TO BE HAPPY::HERE IS WHY








Hello !! Time has gone by since I last drooped to you through this platform. I have to admit that I missed these moments and now thank God I am back and rolling. 

When analyzing the role of those around us towards happiness i realized that for a lot of people, 2022 meant trying times. And divisiveness. We fought with politicians, neighbors, family, friends, the media, men and strangers we’ve never even met, thanks to social media.

AND NOW Our hope for 2023? Perhaps it’s remembering that as much as the people around us can drive us up the wall, no man is an island. It takes all types to make the world go ‘round. And people are meant to be around other people (even those we don’t always agree with).

“Human beings are an ultra-social species — and our nervous systems expect to have others around us,” Emiliana Simon-Thomas, PhD, Science Director of the Greater Good Science Center at The University of California, Berkeley, tells NBC News BETTER. In short, according to biology, neuroscience, psychology, and more, our bodies actually tend to work better when we’re around not alone.

Being lonely has been linked to worse physical and emotional health outcomes and poorer wellbeing. Plus, a lack of social support can directly affects our potential for experiencing happiness, explains Simon-Thomas, who studies the biology of our emotions and thinking. “We’re built to really seek social companionship and understanding.”
Here are all the reasons why:


1. Being around other people makes us healthier.

Physiologically, not having a social support system is actually a source of chronic stress for our bodies, Simon-Thomas explains. Studies show that when people feel lonelier they have higher levels of the stress hormone cortisol. And that type of chronic stress raises risk of cardiovascular disease and other challenges to health and wellness, Simon-Thomas adds. Conversely relationships can encourage behaviors that are good for us, too (like eating right and exercising).

So it makes sense that studies show having fewer social ties is associated with more heart disease, cancer, and impaired immune function, as well as with worse recovery when it comes to those health problems.

Research dating back to the 1970s suggests people with weaker social networks actually die younger (due to any cause) than people who have more extensive social networks. A more recent review of 148 studies concluded that on average having stronger social ties increased likelihood of an individual’s overall survival by as much as 50 percent.
Image result for happy brain

2. Our brains seem to work better when we work together.
There’s a growing body of evidence that suggest our brains actually function better when we’re interacting with others and experiencing togetherness. That’s according to a 2015 review article published by a group of Finnish neuroscientists in the journal Neuron.“Social interaction is among the most complex functions humans (and their brains) perform. Yet, the interaction typically appears surprisingly easy,” the coauthors write in the paper.

Research shows, for example, that listening and participating in a two-person conversation is actually less mentally taxing for the brain than giving or listening to a monologue, even though what we understand about how we process language would suggest otherwise. Other studies show children learn better by interacting with other rather than observing.

3. Psychologically, we prefer to go through life NOT alone.

Psychology says that part of human nature’s default mode is to be social. One theory: people have an innate (and very powerful) need to belong. Some key arguments (published in the journal Psychological Bulletin in 1995) is evidence that shows most people make social ties under most conditions — and most people try to avoid breaking those ties if they can.

Another way to think about it is the social baseline theory, which suggests the human brain expects access to social relationships. That’s because those connections help lower potential risks one might face (think “safety in numbers”) and lessen the amount of effort needed when it comes to a variety of scenarios (if the objective is to build a shelter, there is literally less work for each individual if two people do it).

Experiments have shown that simply holding someone else’s hand lessens an individual’s emotional response in the brain to a perceived threat. (The effect was even greater if the person’s hand you were holding was a spouse.) Another oft-cited experiment found that individuals actually perceived a hill to be steeper if they were standing at the bottom alone compared with when they stood at the bottom with a friend, Simon-Thomas notes. “Just having another person there and present, who you trust and feel safe around makes the world look like a less challenging place,” Simon-Thomas.


Image result for happy black FRIENDS


4. When we’re around people who drive us crazy, we grow.

So what about the coworker who cannot stop preaching his political views? Or your friend’s best friend who you just cannot stand to be around? It’s good when relationships challenge us, says Simon-Thomas.

They can help us extend our status quo and how we see the world, she explains. “These ‘being driven crazy’ moments are truly well thought of as opportunities for growth and transformation, which can ultimately be a more poignant source of sustained happiness.”

That’s because having a diverse variety of emotional experiences — including feeling sad, angry, anxious, or irritated — expands our capacity to feel good, too, she explains. And it’s totally normal for our closest family and friends to be the ones who do that.

The exception is when a relationship’s negatives outshine its benefits. Be wary if a relationship encourages bad habits or causes distress, says Debra Umberson, PhD, Professor of Sociology and Director of the Population Research Center at the University of Texas at Austin. “A bad relationship is worse than no relationship when it comes to health.”

DO IT BETTER: Being grateful for the people around us helps

Simon-Thomas’ advice for reaping the benefits of your social ties: Be grateful for your relationships (including those that challenge you).

Research shows people who are more grateful tend to be happier, tend to be more satisfied in their relationships, tend to be less vulnerable to various physical discomforts, tend to be more resilient when it comes to stress and trauma, and are more well-like by others compared with people who are less grateful, she says. “Make a point of noticing who around you is contributing to the goodness in your life and actually express it by saying thank you.”

And remember, it’s okay to have some “you” time when you need it. We all need time to ourselves to rest, decompress and reflect on whatever’s going on in our lives, Simon-Thomas says. It recharges us for when it is time to face (and embrace) the rest of the world again. 

-KDMULA

Monday, 13 October 2025

TCAA Yakabidhi Kisima cha Maji Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege Dodoma

 

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua, akikata utepe kuashiria ufunguzi wa kisima cha maji safi kilichojengwa kwa ufadhili wa TCAA kwa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege.


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua, akifungua maji kama ishara ya kukabidhi kisima cha maji safi kilichojengwa kwa ufadhili wa TCAA kwa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege, Dodoma. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Mwalimu Cassian Henry.


Muonekano wa kisima cha maji safi kilichojengwa kwa ufadhili wa TCAA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua, akisaini kitabu cha wageni alipowasili Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege.


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua akizungumza muda mchache kabla ya kukabidhi kisima

Afisa Elimu Kata, Bi. Prisca Barnabas akizungumza wakati wa mahafali 


Picha ya pamoja ya timu ya TCAA

Picha ya pamoja na uongozi wa kata, shule na wadau wa elimu

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua, akipanda mti kama ishara ya kuadhimisha miaka hamsini tangu kuanzishwa kwa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege wakitoa burudani ya ngoma wakati wa hafla hiyo


Dodoma, — Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imekabidhi rasmi kisima cha maji safi na salama katika Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege jijini Dodoma, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake iliyotolewa mwaka 2023 na sehemu ya juhudi za kurudisha kwa jamii na kuboresha mazingira ya elimu nchini.


Hafla hiyo ilifanyika sambamba na maadhimisho ya jubilee ya miaka 50 ya shule hiyo na mahafali ya wanafunzi wa darasa la saba, tukio lililohudhuriwa na wazazi, walimu, wanafunzi pamoja na viongozi mbalimbali wa elimu na serikali.


Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua, alisema taasisi hiyo itaendelea kuwa mlezi wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege na kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo hatua kwa hatua, ikiwa ni sehemu ya jitihada za TCAA za kurejesha kwa jamii.


“TCAA itabaki kuwa mlezi wa shule hii. Tutazidi kushirikiana na uongozi wa shule kutatua changamoto mbalimbali taratibu, ili kuhakikisha mazingira bora ya kujifunzia yanadumu. Maji ni uhai, na tunataka kila mwanafunzi hapa ajifunze katika mazingira safi na salama,” alisema Dkt. Mwinyimvua.


Kwa upande wake, Afisa Elimu Kata, Bi. Prisca Barnabas, aliishukuru TCAA kwa mchango huo muhimu na kuahidi kuhakikisha miundombinu ya maji inatunzwa kwa manufaa ya wanafunzi na jamii.

“Tunatoa shukrani za dhati kwa TCAA kwa kujali elimu. Tutahakikisha kisima hiki kinatumika ipasavyo na kudumu kwa muda mrefu,” alisema Bi. Prisca.


Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Mwalimu Cassian Henry, alisema kisima hicho kitarahisisha upatikanaji wa maji na kuboresha mazingira ya usafi na utunzaji wa bustani za shule.


“Kisima hiki ni msaada mkubwa kwetu. Kitatupa uwezo wa kudumisha usafi, kupunguza gharama, na kufanya shule yetu kuwa mazingira bora ya kujifunzia,” alisema Mwalimu Henry.


Katika kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa shule hiyo, Dkt. Mwinyimvua alipanda mti katika eneo la shule kama ishara ya utunzaji wa mazingira na kumbukumbu ya tukio hilo la kihistoria.


Kisima hicho chenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 20, kinatarajiwa kutatua changamoto ya maji kwa wanafunzi, walimu, na wakazi wa jamii inayozunguka shule hiyo.

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA