HABARI MPYA

Monday, 13 October 2025

TCAA Yakabidhi Kisima cha Maji Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege Dodoma

 

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua, akikata utepe kuashiria ufunguzi wa kisima cha maji safi kilichojengwa kwa ufadhili wa TCAA kwa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege.


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua, akifungua maji kama ishara ya kukabidhi kisima cha maji safi kilichojengwa kwa ufadhili wa TCAA kwa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege, Dodoma. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Mwalimu Cassian Henry.


Muonekano wa kisima cha maji safi kilichojengwa kwa ufadhili wa TCAA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua, akisaini kitabu cha wageni alipowasili Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege.


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua akizungumza muda mchache kabla ya kukabidhi kisima

Afisa Elimu Kata, Bi. Prisca Barnabas akizungumza wakati wa mahafali 


Picha ya pamoja ya timu ya TCAA

Picha ya pamoja na uongozi wa kata, shule na wadau wa elimu

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua, akipanda mti kama ishara ya kuadhimisha miaka hamsini tangu kuanzishwa kwa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege wakitoa burudani ya ngoma wakati wa hafla hiyo


Dodoma, — Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imekabidhi rasmi kisima cha maji safi na salama katika Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege jijini Dodoma, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake iliyotolewa mwaka 2023 na sehemu ya juhudi za kurudisha kwa jamii na kuboresha mazingira ya elimu nchini.


Hafla hiyo ilifanyika sambamba na maadhimisho ya jubilee ya miaka 50 ya shule hiyo na mahafali ya wanafunzi wa darasa la saba, tukio lililohudhuriwa na wazazi, walimu, wanafunzi pamoja na viongozi mbalimbali wa elimu na serikali.


Akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TCAA, Dkt. Hamis Mwinyimvua, alisema taasisi hiyo itaendelea kuwa mlezi wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege na kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo hatua kwa hatua, ikiwa ni sehemu ya jitihada za TCAA za kurejesha kwa jamii.


“TCAA itabaki kuwa mlezi wa shule hii. Tutazidi kushirikiana na uongozi wa shule kutatua changamoto mbalimbali taratibu, ili kuhakikisha mazingira bora ya kujifunzia yanadumu. Maji ni uhai, na tunataka kila mwanafunzi hapa ajifunze katika mazingira safi na salama,” alisema Dkt. Mwinyimvua.


Kwa upande wake, Afisa Elimu Kata, Bi. Prisca Barnabas, aliishukuru TCAA kwa mchango huo muhimu na kuahidi kuhakikisha miundombinu ya maji inatunzwa kwa manufaa ya wanafunzi na jamii.

“Tunatoa shukrani za dhati kwa TCAA kwa kujali elimu. Tutahakikisha kisima hiki kinatumika ipasavyo na kudumu kwa muda mrefu,” alisema Bi. Prisca.


Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Mwalimu Cassian Henry, alisema kisima hicho kitarahisisha upatikanaji wa maji na kuboresha mazingira ya usafi na utunzaji wa bustani za shule.


“Kisima hiki ni msaada mkubwa kwetu. Kitatupa uwezo wa kudumisha usafi, kupunguza gharama, na kufanya shule yetu kuwa mazingira bora ya kujifunzia,” alisema Mwalimu Henry.


Katika kuadhimisha miaka 50 tangu kuanzishwa kwa shule hiyo, Dkt. Mwinyimvua alipanda mti katika eneo la shule kama ishara ya utunzaji wa mazingira na kumbukumbu ya tukio hilo la kihistoria.


Kisima hicho chenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 20, kinatarajiwa kutatua changamoto ya maji kwa wanafunzi, walimu, na wakazi wa jamii inayozunguka shule hiyo.

Saturday, 11 October 2025

TCAA YAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KITOFAUTI




Afisa Habari na Uhusiano Mkuu TCAA, Zuhura Lwamo (katikati) akiwasikilza wadau wa usafiri wa anga waliofika kupata huduma katika ofisi ya TCAA kitengo cha taarifa za anga (briefing office)  uwanja wa ndege wa Arusha


Afisa Mtoa Taarifa za Usafiri wa anga wa  TCAA kituo cha uwanja wa ndege wa Arusha, Johneudes Mwombeki (kushoto) akifafanua jambo kwa mdau wa usafiri wa anga aliyefika kupata huduma katika ofisi hiyo


Afisa Habari na Uhusiano Mkuu TCAA, Zuhura Lwamo (katikati) akizungumza na mdau wa usafiri wa anga aliyefika kupata huduma katika ofisi ya TCAA kitengo cha taarifa za anga (briefing office) katika uwanja wa ndege wa Arusha


Meneja wa TCAA kituo cha Uwanja wa Ndege wa Arusha Jackson Ndalu akikabidhi zawadi kama ishara ya kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja



Kaimu Meneja Uhusiano na Mawasiliano TCAA, Ally Changwila (kulia) akiwakaribisha wadau wa usafiri wa anga waliofika Makao Makuu ya TCAA kupata huduma.

Muwezeshaji Rodrick Nabe akitoa mafunzo kwa watumishi wa TCAA kuhusu namna bora ya kutuoa huduma kwa mteja ikiwa ni sehemu wiki ya huduma kwa wateja




Katika kuadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja, Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) inatumia fursa hiyo kusikiliza na kuhudumia wateja mbalimbali wanaofika katika ofisi zake, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha huduma bora na mahusiano mazuri na wadau wake. Maadhimisho haya ya kimataifa yanafanyika kila tarehe 6 hadi 10 Oktoba, yakilenga kuhimiza taasisi na mashirika kutoa huduma bora, zenye ubunifu na zenye kujali mahitaji ya wateja wao.

Katika kipindi hiki, TCAA inapokea na kushughulikia maoni, mapendekezo, na changamoto kutoka kwa makundi mbalimbali ya wateja, wakiwemo marubani, wahandisi wa usafiri wa anga, wanafunzi, na wawakilishi wa mashirika ya ndege. TCAA inaamini kupitia utaratibu huu wa kuwa karibu na wadau, Mamlaka inalenga kuboresha mifumo ya utoaji huduma na kuhakikisha kuwa kila mteja anapata huduma bora, kwa wakati na kwa ufanisi.

Maadhimisho ya mwaka huu yamebeba kauli mbiu isemayo “Mission: Possible – Mpango Umewezekana,” ambapo kwa upande wa TCAA, kauli mbiu hii inadhihirisha dhamira ya kuendelea kutoa huduma bora na zenye ubunifu unaolenga kumuweka mteja katikati ya huduma zote. Kupitia maadhimisho haya, TCAA inathibitisha kujituma kwa watumishi wake katika kufanikisha malengo ya taasisi, kuongeza ufanisi wa huduma, na kudumisha utamaduni wa ubora wa huduma kwa wateja.

Aidha, maadhimisho hayo yaliambatana na mafunzo kwa watumishi wa TCAA kuhusu utoaji wa huduma bora kwa wateja, lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa kutoa huduma zenye ubunifu, weledi, na zinazozingatia mahitaji ya wateja. Bila shaka, kwa TCAA – Mpango Umewezekana.

Saturday, 12 April 2025

TRANSFORM YOUR LEADERSHIP JOURNEY WITH MWALIMU JULIUS NYERERE LEADERSHIP SCHOOL

 



Embark on a transformative leadership journey at the Mwalimu Julius Nyerere Leadership School. Rooted in the timeless values of integrity, unity, and service, our programs are designed to nurture visionary leaders who are ready to shape the future of Africa.

Whether you're an aspiring leader or a seasoned changemaker, our immersive training, mentorship, and pan-African perspective will equip you with the tools to lead with purpose and impact. Join a legacy inspired by one of Africa’s greatest leaders – and become part of the change.

TUGHE TCAA YAPONGEZWA KWA USHIRIKIANO IMARA; YASISITIZWA KUHAMASISHA UANDIKISHAJI WA WANACHAMA WAPYA



Naibu Katibu Mkuu wa TUGHE Taifa, Ndg. Amani Msuya akizungumza wakati wa ufunguzi wa  mkutano mkuu wa mwaka wa cha Chama cha Wafanyakazi wa Serikali kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) uliofanyika jijini Dodoma



Viongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wamepongezwa kwa kuandaa na kuendesha kwa mafanikio makubwa mkutano mkuu wa mwaka, hatua ambayo imewawezesha kujadili kwa kina taarifa mbalimbali za kiutendaji ndani ya chama na kuweka mapendekezo yenye lengo la kuongeza tija ndani ya TCAA.

Akifungua rasmi mkutano huo wa siku mbili uliofanyika jijini Dodoma, Naibu Katibu Mkuu wa TUGHE Taifa, Ndg. Amani Msuya aliwapongeza viongozi wa TUGHE TCAA kwa uendeshaji mzuri wa shughuli za chama kwa namna shirikishi, akieleza kuwa tawi hilo limekuwa mfano bora wa kuigwa na matawi mengine.

"Nawasihi viongozi waendelee kuhamasisha watumishi wengi zaidi kujiunga na TUGHE kwa sababu huo ndio uhai wa chama. Bila wanachama hai, hakuna chama hai. TCAA mmeonyesha njia nzuri, endeleeni kushikamana na kushirikiana," alisema Ndg. Msuya.

Kwa upande wake, Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam, Bi. Sara Rwezaura aliwataka wanachama wa TUGHE TCAA kuwa wavumilivu wakati wa kuwasilisha hoja zao, na kusisitiza kwamba hoja zao ni muhimu na zisikaliwe kimya bali ziwasilishwe kwa mujibu wa taratibu.

Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la TCAA, Bi. Jackline Ngoda aliwashukuru viongozi wenzake kwa kuendelea kudumisha mshikamano ndani ya uongozi na kuahidi kuongeza nguvu katika kuhamasisha watumishi wengi zaidi kujiunga na TUGHE.

Naye Katibu wa TUGHE TCAA, Bw. Shukuru Mhina alisisitiza umuhimu wa mafunzo kwa viongozi wapya wa TUGHE akieleza kuwa ni kupitia mafunzo ndipo viongozi bora hujengwa.

Mkutano huu wa mwaka wa TUGHE TCAA umeendelea kuonesha mfano wa uwajibikaji, mshikamano na ushirikishwaji, hali inayoendelea kuimarisha misingi ya utendaji bora ndani ya taasisi.





Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam Bi. Sara Rwezaula akitoa salamu za TUGHE Mkoa wa Dar es Salaam  wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa cha Chama cha Wafanyakazi wa Serikali kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) uliofanyika jijini Dodoma


Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bi. Jackline Ngoda akizungumza kuhusu namna wanavyoshirikiana na viongozi wa TCAA pamoja na kumkaribisha Mgeni rasmi.


Katibu wa TUGHE Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA),Bw. Shukuru Mhina akifanywa utambulisho wa wajumbe wa mkutano mkuu wa mwaka wa TUGHE tawi la TCAA 



Wajumbe wa mkutano mkuu wa mwaka wa TUGHE tawi la TCAA wakiwasilisha michango wakati wa mkutano






Nsubisi Mwasandende Afisa Elimu Kazi na Mratibu wa Jinsia TUGHE akiwasilisha mada kuhusu mbinu za usajili na kuwatunza wanachama kwa wajumbe wa  mkutano mkuu wa mwaka wa TUGHE tawi la TCAA 




Mgeni rasmi akiwa kwenye picha ya pamoja na Wanachama wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Tawi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).





Friday, 11 April 2025

JIHADHARI NA HIZI KAULI 10 MBAYA KUTAMKA KWA MWENZA WAKO



Mojawapo ya nguzo kuu kabisa ya mahusiano mazuri ni mawasiliano. Mawasiliano mazuri yanahusisha vitu viwili vikubwa, kuwa na ujumbe wa kusema na namna ya kusema ujumbe wako.
Maneno ni kitu hatari sana katika mahusiano yakitumiwa vibaya na yakitumika vizuri ni nguzo kubwa ya mahusiano mazuri na yenye furaha.
Hivyo unatakiwa kupangilia maneno yako unapoongea na mwenza wako ili kupata athari chanya. Ifahamike kuwa maneno mabaya yakisha semwa hayarudi mdomoni na madhara yake yatabaki siku zote hata kama mwenza wako atasema kuwa amesamehe au kusahau.
Maneno yafuatayo ni hatari kwa kuwa yanaleta madhara makubwa moyoni mwa mlengwa na ni vyema kuzuia kuyatamka kwa namna yoyote ile.

Maneno 10 Mabaya Ambayo Hutakiwi Kusema Kwa Mwenza Wako:

  1. Maneno Ya Matusi

Maneno kama “mjinga” au “mpumbavu” yasitumike kwa mwenza wako hata kama yana ukweli ndani yake. Japo ujinga ni kutofahamu kitu fulani lakini neno hili linaleta majeraha kama likitoka kwa mwenza. Hasa kama linatoka wakati wa ugomvi au kutofautiana.
Useseme maneno mabaya yanayomshusha mweza wako mfano kuhusu mwonekano mbaya wa mwenza wako kama “sura mbaya”,”Mnene kama nguruwe” n.k
  1. “Nakuchukia”

Chuki ni kitu kikubwa sana,kwa kweli huwezi kuishi na mtu ambaye unamchukia. Hutakiwi kumtamkia mwenza wako neno hili. Unaweza kuchukia tabia yake lakini si yeye mwenyewe. Njia nzuri ni kusema kuwa “Nachukia au sipendi tabia yako ya kuchelewa kurudi nyumbani” au maneno yanayofanana na hayo.
  1. “Ameiga Tabia Zako”

Wazazi wanatabia ya kurusha lawama kwa wenza wao pale watoto wanapokuwa na tabia mbaya. Utasikia mzazi mmoja akisema kwa mtoto “Tabia za mama yako hizi” au “Tabia za baba yako” pale mtoto anapoonesha tabia mbaya. Maneno haya hayafai kutumika katika familia kwakuwa yanashambulia nafsi ya mwenza wako.
  1. Kumfananisha Tabia Mbaya Za Mwenza Na Wazazi Wake

“Tabia zako kama mama yako”, au “..kama baba yako” maneno yanayomfananisha mwenza wako na wazazi au familia anakotoka yanachokoza sana na huweka vidonga kwa muda mrefu moyoni na yaepukwe.
  1. “Acha!Nitafanya Mwenyewe”

Katika mahusiano kusaidiana ni jambo la kawaida na muhimu,maneno mabaya ya namna hii yanamvunja moyo mweza wako kutaka kufanya jambo kwako siku nyingine na linaleta utengano na kuvunjika kwa upendo.
  1. Maneno Mabaya Ya Kukatisha Tamaa

“Hutaweza” ,”Hutafanikiwa” n.k yanavunja moyo kwa mwenza wako na kurudisha nyuma maendeleo.
Ni muhimu kwa wenza kupeana moyo na kusaidiana ili wote muende mbele kwa pamoja. Umoja ni nguvu.
  1. “Mtoto Wangu”

Itambulike kuwa hakuna mtoto wa mtu mmoja,wenza wote wawili wana haki na wajibu sawa juu ya mtoto wao. Najua mila na desturi zimetufundisha tofauti juu ya haki juu ya mtoto kwa wazazi wawili lakini ukweli ni kuwa wazazi wote wana nafasi na haki sawa kwa mtoto wao.
  1. “Haya Yote Ni Makosa Yako”

Lawama hazijengi bali zinabomoa. Lawama zinavunja moyo kwa mwenza wako. Pale panapotokea shida au matatizo kati yenu ni vyema kuyachukua kama yenu wote na mtafute suluhisho kwa pamoja.
  1. Kutolea Mifano Mahusiano Ya Zamani

Usithubuthu kumfananisha mwenza wako na mpenzi wa zamani hata kama wazamani alikuwa bora zaidi kwa vigezo vyako. Mfano “John alikuwa ananitoa sana,lakini wewe hufanyi hivyo” au “John alikuwa anapenda sana chakula hiki”
Kama ikitokea umegusia mahusiano ya zamani jaribu kuonesha haya uliyopo sasa ni Bora zaidi ya yote yaliyopita mfano "wewe ni bora kuliko wote" au sijapata kama wewe" hii inatia zaidi na kumfanya mwenza wako kujiona wa pekee.
  1. Maneno Juu Ya Kuachana

Usitumia maneno yanayoashiria nia ya kuachana,yanaondoa imani juu ya masiha ya mahusiano yenu.
Mfano “Kwa mtindo huu mimi nafikiri hatutafika mbali”
Mwenza wako ataanza kujiandaa kuachana na hatajiachia kwa asilimia zote kwa mapenzi na mipango ya pamoja. Maneno haya yanajenga utengano taratibu ndani ya moyo wako na wa mwenza wako.

Mwisho

Kama nilivyosema mwanzoni,mawasiliano ni nguzo ya mahusiano mazuri kati ya weza wawili. Ni kitu ambacho kila mmoja anatakiwa kujifunza na kukitilia maanani hasa kwa kujua mahusiano ya mke na mume yana changamoto kubwa kutokana na utofauti wa kihisia na kitafakuri kati ya mke na mume.
Mwanamke na mwanaume wanaonekana kama viumbe tofauti toka sayari tofauti kutokana na namna zao tofauti za kuwasiliana na kuelewa ujumbe toka kwa mwingine.
Busara za kuchambua nini cha kusema na kipi kuacha kutasaidia sana kuboresha mahusiano na mwenza wako
Nini changamoto zako na mwenza wako katika mawasiliano? Maneno mabaya yapi ambayo yanakukera kuambiwa na mweza wako na unafikiri si vyema kuyatumika kwa weza ukiacha haya? Tafadhari shiriki kujadili kwa kuandika katika kisanduku hapa chini.
Asante na nawatakia mahusiano na mwasiliano mema.

Thursday, 10 April 2025

WATUMISHI WA TCAA WAPONGEZWA KWA BARAZA LA WAFANYAKAZI LENYE TIJA





Msajili wa Hazina, Bw. Nehemia Mchechu akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la TCAA wakati wa kufungua kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Takwimu House Dodoma.





Watumishi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) wamepongezwa kwa kuwa moja ya taasisi za umma zinazoendesha Baraza la Wafanyakazi lenye tija, ambalo limeendelea kuwa kichocheo cha maamuzi makubwa ya kuboresha huduma za usafiri wa anga nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Msajili wa Hazina, Bw. Nehemia Mchechu, wakati wa ufunguzi wa Baraza la Pili la Wafanyakazi la TCAA kwa mwaka wa fedha 2024/2025, lililofanyika Aprili 10, 2025, jijini Dodoma.

Bw. Mchechu alisisitiza umuhimu wa vikao vya Baraza katika kuimarisha misingi ya demokrasia sehemu za kazi na kuwahamasisha wajumbe kuhakikisha wanawasilisha mrejesho kwa watumishi wenzao waliowawakilisha ili kujenga mshikamano na ufanisi katika kutekeleza majukumu yao.

"Baraza hili si tu jukwaa la mijadala, bali ni daraja la kuelekea maboresho ya kweli ya mazingira ya kazi. Mnapaswa kulitumia kama chombo cha kuleta mabadiliko chanya, lakini pia kuhakikisha kila mtumishi anapata fursa ya kushiriki katika safari ya maendeleo ya taasisi," alisema Bw. Mchechu.

Aidha, aliipongeza menejimenti ya TCAA kwa kujenga mazingira mazuri ya kazi na kuwezesha ufanisi wa Baraza hilo, akisema kuwa hatua hiyo ni mfano wa kuigwa na taasisi nyingine.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Bw. Salim Msangi, akimkaribisha Bw.Mchechu alieleza kuwa Mamlaka itaendelea kuboresha mazingira ya kazi ili kila mtumishi aweze kutimiza wajibu wake kwa weledi na kuisukuma mbele sekta ya usafiri wa anga.

"Menejimenti inatambua mchango wa kila mmoja wenu. Ni muhimu kila mtumishi afahamu kuwa TCAA inajengwa kwa juhudi za pamoja. Naomba tushirikiane, tusaidiane inapobidi, kwa kuwa tunalenga kuhakikisha malengo ya taasisi na Serikali kwa ujumla yanafikiwa na huduma bora inatolewa kwa Watanzania," alisema Bw. Msangi.

Baraza la wafanyakazi lina lengo la kuendeleza mawasiliano ya wazi kati ya menejimenti na watumishi, pamoja na kujadili mikakati ya kuboresha huduma, mazingira ya kazi, na ufanisi wa taasisi.

Katika kuimarisha uelewa wa maendeleo ya sekta ya anga, wajumbe wa Baraza pia watapata fursa ya kufanya ziara ya kutembelea na kujionea hatua ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato, uliopo jijini Dodoma. Ziara hiyo inalenga kuwapa watumishi uelewa wa kina kuhusu juhudi za serikali na mchango wa TCAA katika kukuza miundombinu ya usafiri wa anga nchini.





Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Bw. Salim Msangi akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la TCAA wakati wa ufunguzi wa kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Takwimu House Dodoma.



Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la TCAA wakiwa katika picha za pamoja na meza kuu






Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la TCAA kwa pamoja wakiimba nyimbo ya mshikamano 

Wednesday, 9 April 2025

JIFUNZE JINSI YA KUISHI NA FURAHA MAISHANI MWAKO




Mpendwa msomaji wa FUNGUKA LIVE ikiwa tunaelekea tamati ya mwaka wa 2016 nimeguswa kuandika makala hii muhimu kwani naamini tangu tuuanze huu mwaka tayari tumepita katika hali tofauti na sasa ni vyema kabla ya mwaka kuisha (kwa Neema Za Mungu) tukajifunza hili.

Leo tutaangalia jinsi inavyokupasa uyaachie mambo yanayokusumbua, ili uishi kwa furaha. Tutaangalia jinsi ya kuachana na mambo mbalimbali tunayokutana nayo katika maisha ili kuweza kupata amani na utulivu katika mioyo yetu.

Kumbuka kuwa kama una tabia ya kuachana na ya maumivu na huzuni unayokabiliana nayo, utakuwa na maisha mazuri, lakini kinyume cha hapo, utaendelea kuwa mtu asiyekuwa na furaha siku zote.

Na pia ufahamu kuwa, kila mmoja wetu hukabiliana na changamoto mbalimbali katika sehemu fulani ya maisha yake, kama vile, hali ya huzuni au kukataliwa lakini njia nzuri ya kuishi vizuri ni kuwa jasiri katika kuikabili hali hiyo.

Japo wapo watu wengine hudhani, kwa kuwa wao ni washika dini sana, hali ya huzuni, kuhangaika, kukata tamaa haitawapata, la hasha! Kila mmoja anapatwa na hali hiyo, ila ni uamuzi wako kuchagua ni jinsi gani unapenda uwe, kuwa na furaha ama kutokuwa nayo.

Pia ukiangalia watu wengi ambao hawana furaha, hukabiliwa na magonjwa mbalimbali. Huweza kuwatambua kwa kuwaangalia muonekano wao kiafya, vile vile hupatwa na maradhi kama shinikizo la moyo, moyo kudunda kwa nguvu, kupooza na hata wakati mwingine kuugua kansa ambayo huzalishwa na hali ya msongo wa mawazo.

Kwa upande mwingine wa maisha haya tunayoyaishi, ujue kuwa nayo yana kanuni zake, kama unataka watu wakutendee mambo mema, nawe pia watendee yaliyo mema, kwa kila jambo unalotenda.Ingawa pale unapokosa kutendewa wema ingali wewe umetenda hili huzaa huzuni na maumivu (Usife moyo mazuri yako yanakuja).

Kwa kila tendo jema, kuna mwitiko ulio mzuri, kinyume cha hapo hutabaki kuumia na kukosa furaha maishani. Wema wako unaowatendea wengine, ndivyo hivyo nawe utapokea katika maisha yako kutoka kwao.

Tiba ya kuishi maisha ya furaha ni hii ‘kuwa mzuri, kuwa mwema, usiwe mbinafsi. Watendee wengine vile unavyopenda wakutendee wewe’.
Kama kweli umedhamiria kupata furaha ya kutosha maishani, tumia kanuni hiyo ya maisha na kuifanyia kazi.

Kama unataka kuwa rafiki wa watu, nao wawe rafiki zako. Kuwa rafiki kwao na kama umezungukwa na watu wasio wazuri kwako, wabadili wawe watu wazuri kwa kuonyesha wema wako kwao, haijalishi jinsi watakavyokuchukulia.

Je, unadhani utawabadilishaje ili wawe watu wazuri? Ni kwa kushirikiana nao katika mambo yaliyo mema na kuwajali. Inawezekana wanaweza wasikukubali kirahisi, lakini jitahidi kuwa mwema kwao, bila kujali wanachokisema wala kukinong’ona.

Hebu tuangalie mfano wa mama mmoja, aliyekuwa ameolewa lakini hakuwa na furaha na mumewe, kwa kuwa kila alichokifanya mumewe huyo alikikosoa.

Mwanamke huyo aliamua kutafuta msaada kwa kiongozi wake wa dini na kumweleza kuhusu mumewe kwamba kila aliporudi nyumbani alikuwa na hasira na kukosoa kila jambo aliloliona limefanyika.

Lakini mama huyo, alipoomba ushauri, aliambiwa kuwa, inawezekana yeye ndiye chanzo cha yote kabla ya kumsema mumewe, ni vema akajiangalie yeye kwanza, jambo alilokubaliana nalo na kulifanyia kazi, baada ya muda, mumewe alibadilika. Furaha ikatawala nyumbani kwao.

Mwanamke huyo alisema, aliamua kubadilika kwa kumjali mumewe na kuwa karibu naye, bila kujali vile alivyokuwa akimtenda na kwamba kila mumewe huyo aliporudi nyumbani, na kuanza kukosoa kama alivyozoea, kwa kuwa mwanamke alikubali kubadilika, alijitahidi kumhudumia kwa upendo, kumpatia chakula, juisi na kumpa maneno matamu, bila kujali jinsi alivyokuwa akifoka kwa hasira.

Alisema aliendelea kuwa karibu na mumewe kila siku na mwishoni mumewe huyo alibadilika tabia yake ile aliyokuwa nayo. Kama unataka kuyabadili mazingira magumu unayokutana nayo, ni vema ukaanza kubadilika wewe kwanza.

Fikiri juu ya hili. Je, ni jambo gani linalotufanya kuwatendea watu mambo mema? Ni kwa kuwa, nasi tunapenda kutendewa mambo mema pia? Kamwe tusiruhusu hali ya chuki na hasira katika maisha tunayoyaishi. Mbaya zaidi hali ya hasira zilizofichika ndani vinginevyo utapata maumivu na majeraha yaliyofichika ambayo yanahitaji kuponywa.

Majeraha hayo yaliyofichika hukusababishia hasira, ugomvi ama hali yoyote ambayo hupendi utendewe na mtu mwingine. Baadhi ya dalili zinazomfanya mtu aonekana kama ana majeraha yaliyofichika ni maneno yake, mwonekano na vitendo vyake.

Sasa basi njia ya kukabiliana na maumivu ya ndani uliyonayo ni kuyasahau na kutokumbuka mambo uliyowahi kutendewa. Watu wengi wanakosa furaha ya kweli, kwa kuwa wamekuwa wakikumbuka jinsi walivyotendewa na baba au mama yake, alipokuwa mdogo, mke au mme wake alivyomtendea siku za nyuma, kwa kuwa wanashindwa kusamehe, miaka inapita huku maumivu hayo yakiwa yanaendelea.

Usilaani. Kamwe usiruhusu maumivu yakakufanye mtu mwenye uchungu, jaribu kusahau, kumbuka kuwa, huwezi kusahau maumivu yaliyokupata kama utakuwa unayakumbuka kumbuka.
Ni vyema tukajiona wa thamani na kuamini kuwa tunastahili kuishi na kuwa na furaha, Amini amani na furaha ya kweli ni Kutoka  kwa Mungu hivyo wanadamu hawana haki ya kukufanya uishi kwa huzuni.
FURAHA NI HAKI YAKO
Unaweza  kubofya na kupitia makala zetu - MAHUSIANO makala nyingine- HAPA

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA