TCAA YAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KITOFAUTI


Muwezeshaji Rodrick Nabe akitoa mafunzo kwa watumishi wa TCAA kuhusu namna bora ya kutuoa huduma kwa mteja ikiwa ni sehemu wiki ya huduma kwa wateja
Katika kipindi hiki, TCAA inapokea na kushughulikia maoni, mapendekezo, na changamoto kutoka kwa makundi mbalimbali ya wateja, wakiwemo marubani, wahandisi wa usafiri wa anga, wanafunzi, na wawakilishi wa mashirika ya ndege. TCAA inaamini kupitia utaratibu huu wa kuwa karibu na wadau, Mamlaka inalenga kuboresha mifumo ya utoaji huduma na kuhakikisha kuwa kila mteja anapata huduma bora, kwa wakati na kwa ufanisi.
Maadhimisho ya mwaka huu yamebeba kauli mbiu isemayo “Mission: Possible – Mpango Umewezekana,” ambapo kwa upande wa TCAA, kauli mbiu hii inadhihirisha dhamira ya kuendelea kutoa huduma bora na zenye ubunifu unaolenga kumuweka mteja katikati ya huduma zote. Kupitia maadhimisho haya, TCAA inathibitisha kujituma kwa watumishi wake katika kufanikisha malengo ya taasisi, kuongeza ufanisi wa huduma, na kudumisha utamaduni wa ubora wa huduma kwa wateja.
Aidha, maadhimisho hayo yaliambatana na mafunzo kwa watumishi wa TCAA kuhusu utoaji wa huduma bora kwa wateja, lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa kutoa huduma zenye ubunifu, weledi, na zinazozingatia mahitaji ya wateja. Bila shaka, kwa TCAA – Mpango Umewezekana.






0 comments:
Post a Comment