Tuesday 25 March 2014

UN yalaani Misri kwa hukumu ya kifo



Mahakama kuu Misri
Umoja wa Mataifa umelaani kitendo cha Misri kuwahukumu kifo zaidi ya watu miatano ikisema kuwa ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa za haki za binadamu.
Umoja huo umesema kuwa idadi ya watu waliohukumiwa Jumatatu, ndio idadi kubwa ya watu kuwahi kuhukumiwa kifo kwa wakati mmoja katika miaka ya hivi karibuni.
Mawakili wa utetezi wamesusia kesi ya pili ya watu wengine karibu miasaba wafuasi wa Morsi wanaokabiliwa na tuhuma sawa na zile zilizowakabili watuhumiwa wa kwanza.
Wamlalamikia kile wanachosema ni mahakama kukosa kufuata utaratibu unaofaa.
Kesi ya wafuasi wengine 682 waliosalia ilianza kusikilizwa mapema leo lakini ikaahirishwa baada ya muda mfupi huku jaji akisema kuwa hukumu itatolewa mwezi ujao.
na BBC

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA