WASANII WENGI WA KIKE WA BONGO MOVIE WANAVUTA BANGI,MSANII MWENZAO AKIRI.
Akiwa katka mahojiano na mwandishi wa Swahili Tz msanii mwenye heshima katika kiwanda cha bongo movies Yobnesh Yusuph 'Batuli' aliweka wazi kuwa wasanii wengi wa kike ni watumiaji wazuri na ndio wanaongoza kwa uvutaji bangi kuliko wakiume.
Batuli alisema kuwa wasanii wengi wa kike wamekuwa wakitumia sana kilevi hicho cha marijuana ama ganja hasa wanapokuwa kwenye magari yao,nyumbani,wakiwa location na wengine hujiiba kwa kujificha katika sehemu zisizoonekana lakini harufu ya mmea huwaumbua pindi wanaporejea.
''Wanawake ndio nimekuwa nikiwashuhudia sana kwa sababu mara nyingi nimekuwa nikitembelea katika vyumba vyao wanavuta sana BANGI hata muda mwingine utawakuta wamejifungia kwenye magari wakivuta,wengine hujitahidi kujificha lakini harufu ndio huwa inawaumbua mara nyingi."
0 comments:
Post a Comment