Saturday 15 March 2014

Watafuta kazi wakutana na kifo

 15 Machi, 2014 - Saa 15:02 GMT
Polisi nchini Nigeria
Inaarifiwa kuwa watu kadhaa wamekufa na wengi kujeruhiwa katika msongamano kwenye uwanja wa michezo wa taifa katika mji mkuu wa Nigeria, Abuja.
Majeruhi kadhaa wamepelekwa hospitali lakini maafisa hawana hakika watu wangapi wamekufa.
Mwandishi wa habari mmoja wa Ufaransa anasema aliona maiti saba.
Hayo yalitokea wakati wa kuajiri watu katika idara ya uhamiaji ya Nigeria.
Maelfu ya watu walijitokeza kufanya mtihani wa ajira - inaarifiwa mkanyagano ulitokea walipojaribu kufika katikati ya uwanja.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA