Friday, 16 May 2014

MVUA YAWAPIGANISHA MADEREVA MOSHI


Stori na KD MULA
 Dereva wa dala dala ambayo nambari zake hazikufahamika alijikuta katika timbwili zito baada ya kuvamiwa na dereva wa piki piki almaarufu boda boda leo wakati akiwahi kupaki gari katika stendi ya dala dala eneo la majengo kwa mtei mjini moshi.
Madereva hao ambao majina yao haya kupatikana mapema walishindwa kuzuia hasira zao na kutupiana makonde asubuhi asubuhi huku wakiwapa mzigo mashuhuda burudani ya bure kwa umahiri waliounoesha.





NGOMA INOGILE
 
Akisimulia kisa hiki shuhuda alietutumia habari hii alisema kisa cha ugomvi alisema
“huyu dereva wadala dala alikuwa akiwahi kupaki gari kwenye kilo na kama ilivyo wakati wa masika ALIMMWAGIA MAJI dereva wa boda boda aliekuwa amejiegesha pembeni na alipotakiwa kusimama aliendelea na safari sasa alipopaki tu ndio jamaa akamvaa na kuanza kutupiana makonde”.
MASHUHUDA WAKIENDELEA KUFAIDI SHOW


WADAU WAJA KUAMUA UGOMVI
Baada ya kuamuliwa na mpaka mwandishi wetu anaondoka eneo la tukio madereva hawa kila mmoja alikuwa akielekea kituo cha polisi cha majengo SIJUI WALIPOKUTANA HUKO NINI KILITOKEA…..
PICHA NA MOHAMED MGANGA

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA