CHEKI HAPA MPIGHA DEBE ALIVYO VUNJA REKODI YA MWAKA KWA KUWA'SUPRISE' WATOTO YATIMA
07:29 |
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mpigadebe maarufu katika kituo cha mabasi cha mbalizi wilayani mbeya amenunua mbuzi wawili na bidhaa nyingine za aina mbalimbali zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni moja na kuzipeleka kwenye vituo vya watoto yatima kama zawadi huku akiwaasa watoto hao kutoshawishika kwenda kupiga debe kwenye vituo vya mabasi.
Mpigadebe maarufu katika kituo cha mabasi cha mbalizi, Anganile Mwamuluma Andrea ambaye amefanya kazi hiyo kwa zaidi ya miaka 20 ameushangaza umma wa wakazi wa mbeya baada ya kuamua kununua mbuzi wawili, mchele, maharagwe, sabuni, mafuta ya kupikia na mahindi na kupeleka bidhaa hizo katika vituo viwili vya watoto yatima ambako amezitoa kama zawadi kwa watoto hao, huku akiwaasa kutoshawishika kujihusisha na kazi ya kupiga Debe kwenye vituo vya mabasi.

Walimu wa watoto hao wameeleza kushtushwa na kitendo cha mpigadebe huyo, lakini wakasema kuwa ni mfano Bora wa kuigwa kwa vijana wanaofanikiwa kukumbuka mazingira walikotoka, huku wakiwahimiza wazazi kuongeza upendo kwa watoto wao ili kupunguza wimbi la watoto wanaoishi katika mazingira magumu nchini.
Baadhi ya watoto ambao wamepokea msaada huo, wamemshukuru mpigadebe huyo na kuwataka watu wengine kupata funzo la kuthamini na kuwapenda watoto ikiwa ni pamoja na kuwaandalia mazingira mazuri ya kujitegemea.
-ITV
Related Posts:
SERIKALI YATENGA BILLIONI 60 KUFUFUA GENERAL TYRES ARUSHA Shillingi Billioni 60 zinategemea kutumika kufufua kiwanda ya matairi cha General Tyres kilichopo Jijini Arusha ambacho kimesharudi mikononi mwa… Read More
NEC YASEMA ELIMU YA MPIGA KURA HAIKUWAFIKIA BAADHI YA WANANCHI NCHIN Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini NEC imebainisha kwamba, ukosefu wa elimu ya kutosha kwa Wapiga Kura, ulisababisha mapungufu mbalimbali kujitokeza … Read More
TANZANIA KUENDELEZA UTAFITI WA BIOTEKNOLOJIA Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Uvuvi, Dk. Florens Turuka (kulia), akizungumza na watafiti wa kilimo Dar es Salaam leo asubuhi, wa… Read More
DC MAKONDA ATOA SIKU 20 WENYEVITI WOTE WA SERIKALI ZA MITAA KINONDONI JIJINI DAR ES SALAAM WAPEWE RAMANI ZA MITAA YAO Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (kulia), akizungumza na Watendaji na Viongozi wa Serikali za Mitaa wa wilaya hiyo kwenye mkutano ul… Read More
DUNIA YAAGIZWA KUMALIZA UKEKETAJI 2030 WATENDAJI wakuu wa mashirika mawili makubwa ya Umoja wa Mataifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA) na S… Read More