HATARI...POLISI WAKAMATA ZANA ZA MILIPUKO HUKO TANGA, ZILIKUWA ZIKITOKEA NIGERIA
09:06 |
Jeshi la Polisi mkoani Tanga limewakamata kisha kuwatia mbaroni raia wawili wa kigeni kutoka Nigeria wakiwa na zana za milipuko inayotumiwa katika vitendo vya kigaidi.
Kamanda wa Polisi mkoani Tanga kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi Fraisser Kashai amesema watuhimiwa hao waliotambulika kwa majina ya Kenneth Ekeneh Luodo na Amick Bonniface Aje ambao wamekamatwa katika kijiji cha kigwasi kilichopo kata ya mashewa wilayani Korogwe ambapo walikutwa kwa mwenyeji wao aliyetambulika kwa jina la Frank ambaye alitoroka baada ya operesheni hiyo.
Amesema zana hizo ambazo pia hutumika kuvunja miamba na majengo watuhumiwa walikuwa wamezihifadhi katika mabegi ndipo jeshi la Polisi walipowakamata na kuwatia mbaroni kwa ajili ya upelelezi zaidi huku jitihada za kumtafuta mwenyeji wao Frank zikiendelea.
Katika tukio lingine kamanda Kashai amesema mtu mmoja Michael Charle amekamatwa akiwa na risasi 39 za silaha za kivita ambazo anadai kuwa anafanya biashara ya kuuza risasi kinyume cha taratibu ambazo amedai kuwa ametoka nazo Monduli mkoani Arusha kwenda mkoani Morogoro.
CHANZO:ITV
Related Posts:
MBATIA AIBOMOA BAJETI 2015/2016,ASEMA NI BAJETI LIPUA LIPUA Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, James Mbatia KAMBI Rasmi ya Upinzani Bungeni kupitia kwa Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, James Mbatia, imesom… Read More
RAIS JAKAYA KIKWETE, MAKAMU WAKE DKT. BILAL WAWAONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA ALIYEKUWA MBUNGE WA GEITA, VIWANJA VYA KARIMJEE, DAR. Rais Jakaya Kikwete, mkewe Mama Salma, wakitoa heshima za mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Geita, mare… Read More
DK SHEIN AISHUKURU CHINA KWA MISAADA RAIS wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ameishukuru Serikali ya China kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha sekta ya afya ikiwa n… Read More
MUFTI SIMBA KUZIKWA SHINYANGA Dar es Salaam. Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti, Issa Shaaban Bin Simba amefariki dunia jana katika Hospitali ya TMJ, Dar es Salaam alikokuwa a… Read More
WASHINDI WA TUZO ZA TANAPA 2014 WAKABIDHIWA TUZO JIJINI MWANZA Meneja Mawasiliano wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) ,Pascal Shelutete akitoa neno la ukaribisho katika hafla ya utoaji tuzo kwa wanah… Read More