Sunday, 2 November 2014

AGUERO AIUA MANCHESTER UNITED ,MAN CITY IKZIDI KUPAA


Ligi kuu ya soka nchini England imeendelea hii leo kwa michezo miwili iliyopigwa huko jijini Manchester na jijini Birmingham .
Katika mchezo wa kwanza Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Manchester City waliwafunga mahasimu wao wa jadi Manchester United kwa bao moja bila katika mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Etihad .
Bao pekee lililoamua mchezo huo lilifungwa na mshambuliaji raia wa Argentina Sergio Kun Aguerro ambaye alimalizia pasi ya Gael Clichy .
aguerro

United katika mchezo huo ilimaliza ikiwa pungufu baada ya mlinzi Chris Smalling kuonyeshwa kadi nyekundu mapema kwenye kipindi cha kwanza .
Matatizo ya United hayakuishia hapo kwani baadaye mlinzi wa kimataifa wa Argentina Marco Rojo alilazimika kutolewa nje baada ya kuumia bega lake .
Huu ni ushindi wa nne mfululizo ambao City inaupata mbele ya United huku Sergio Aguerro akiendelea kuwaumiza mashetani wekundu akiwa amefunga mabao matano kwenye michezo sita dhidi ya United .

Related Posts:

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA