Thursday 16 April 2015

WAHAMIAJI 400 WAHOFIWA KUFARIKI DUNIA WAKIJARIBU KUINGIA ULAYA ISIVYO HALALI


Zaidi ya wahamiaji 400 toka Afrika waliokuwa wakijaribu kuingia barani Ulaya wanahofiwa kuwa wamefariki dunia baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama walipokuwa wakitokea nchini Libya kuelekea Ulaya. 

Inaripotiwa kuwa zaidi ya wahamiaji 8,000 walikuwa wakijaribu kuvuka bahari ya Mediterranean mwishoni mwa wiki. 

Boti hiyo iliyozama ilikuwa na wahamiaji 550, na ilizama saa 24 baada ya kuondoka pwani ya Libya. 

Manusura 150 waliokolewa na kukabidhiwa katika mamlaka husika nchini Italia.
Mfanyakazi wa shirika la msalaba mwekundu akiwa amembeba mtoto mchanga wa mmoja wa wahamiaji huku akiwa amefunikwa kwa blanketi kumuepusha na baridi kali baada ya kupokelewa katika kisiwa cha Cicilian
                                                                 Baadhi ya wahamiaji wakiwa katika boti






0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA