MKUU WA WILAYA MOSHI AZINDUA RASMI SHINDANO LA MISS KILIMNAJARO 2016
Baadhi ya warembo ambao ni washiriki wa Miss Kilimanjaro 2016 wakifungua vinywaji aina ya "shampein" kuashiria uzinduzi wa shindano hilo kwa mwaka huu |
Mmoja kati ya waaandaji wa hafla hiyo akimminia kinywaji Mkuu wa wilaya Mh Novatus Makunga aina ya "shampein" iloyofunguliwa kama ishara ya kuwa shindano limefunguliwa rasmi |
Jana,Mkoa wa Kilimanjaro kushuhudia hafla ya uzinduzi wa shindano la kumsaka mlimbwende atakayewakilisha mkoa huo katika ngazi ya Miss Tanzania uliohudhuriwa na mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga na kuzinduliwa rasmi na Mkuu wa wilaya ya Moshi mjini Mh. Novatus Makunga .
Washiriki wa Miss Kilimanjaro 2016 wakionesha umahiri wao katika kucheza mbele ya wageni waliohudhuria halfa hiyo |
Baadhi ya wadau waliohudhuria hafla hiyo wakifurahia burudani iliyokuwa ikitolewa na washiriki wa Miss Kilimanjaro 2016 |
Muandaaji wa Miss Kilimanjaro 2016 Bi.Dotto Sang'wa akitoa utangulizi katika hafla hiyo |
“Tumejipanga kuhakikisha tunabadili muono wa jamii katika tansia ya urembo kwa kuhakikisha kuwa warembo wetu( wanaoshiriki shindano kwa mkoa wa Kilimanjaro) wanapata mafunzo bora kabisa wakiwa kambini hasa tukilenga wakaitumikie jamii kwa dhati na kwa hili tunahitaji ushirikiano wenu sana” aliongeza Bi. Dotto.
Hafla hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Salonero nje kidogo ya mji wa Moshi ilihidhuriwa na mstahiki meya wa manispaa ya Moshi mjini Raymond Ngoya , Kamanda wa Polisi wilaya ya moshi Afande Omary Ntungu pamoja na wawakilishi wa kampuni mbalimbali.
Mkuu wa wilaya ya Moshi mjini Mh. Novatus Makunga akitoa hotuba fupi kabla ya zoezi la uzinduzi wa shindano hilo
|
Akizungumza wakati anazindua,Mh Novatus Makunga alieleza kuwa sasa umefika wakati wa wanakilimanjaro kumuunga mkono muandaaji ili kuhakikisha Kilimanjaro kwa ujumla inafika mbali katika mashindano ya ulimbwende katika ngazi zote.
Aidha wakati akielezea historia fupi ya mashindano ya ulimbwende kitaifa pamoja na kukabidhi katiba ya uendeshwaji wa miss Tanzania kwa muandaaji wa shindano hili mkoa wa Kilimanjaro, mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga alisema miongoni mwa jambo la kustaajabisha ni kwamba asilimia kubwa ya washindi wa miss Tanzania kitaifa wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro.
Muandaaji wa Miss Kilimnjaro 2016 Bi. Dotto Sang'wa akionesha katiba kwa wageni waliohudhuria hafla hiyo
|
0 comments:
Post a Comment