Thursday 19 May 2016

MABAKI YA NDEGE YA EGYPTAIR YAONEKANA UGIRIKI


Mabaki ya ndege ya EgyptAir MS804 iliyoanguka yameonekana kusini mwa kisiwa cha Ugiriki cha Karpathos, Shirika la Anga la Misri limethibitisha.Ndege hiyo aina ya Airbus A320 ilikuwa ikitokea Jijini Paris kwenda Cairo ikiwa na abiria 66 na wahudumu wakati ikianguka.

Wizara ya usafirishaji jijini misri zimethibirisha kupatikana kwa mabaki ya  ndege iliyokuwa imepotea iliyokuwa ikitoka kairo kuelekea misri MS 804 karibu na kisiwa cha Karpathos ripoti za kiwanja haicho kilithibisha kupatikana na mabaki ya ndege hiyo hivyo basi kampuni hiyo imetoa salamu za rambirambi kwa familia ya watu waliokuwepo na wahudumu wa ndege hiyo.

 Kwa sasa kundi la wachunguzi wa Misri wakishirikiana na wenzao wa Ugiriki wanaendelea kutafuta mabaki mengine ya ndege hiyo.
 Ndege hiyo ilikuwa imepaa kutoka uwanja wa ndege wa Charles de Gaulle, Paris ikiwa na raia 15 wa Ufaransa. Ndege hiyo pia ilikuwa na raia 30 wa Misri, raia 2 wa Iraq na raia mmoja mmoja kutoka Uingereza, Canada, Ubelgiji, Kuwait, Saudi Arabia, Algeria, Sudan, Chad na Ureno.Awalia rais wa Ufaransa Francois Hollande alikuwa amesema kuwa ndege hiyo ilianguka.



Makamu wa rais wa Misri Ahmed Adel ameliambia shirika la habari la CNN operesheni ya uokoaji imeanza kufanya jitihada za kuyafikia mabaki ya ndege hiyo.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA