Sunday, 12 June 2016

AL-SHABAB LADAI KUWAUA WAPELELEZI WA KENYA NA US

Image result for al shabaab
Kundi la wanamgambo nchini Somalia, al-Shabab, wanasema wamewaua watu watatu kwa kuwapiga risasi na kumchinja shingo mwingine, baada ya kupatikana na hatia ya kuwa majasusi wa mashirika ya ujasusi ya Kenya na Marekani.
Mauaji hayo yalitekelezwa mbele ya umati wa watu katika mkoa wa Bakool.
Image copyright
Image result for Ahmed Godane
Ahmed Godane
Image caption
Kulingana na taarifa ya radio ya al-Shabaab, mwanamume mmoja aliyeuawa ni Mohamed Aden Nur, ambaye anashutumiwa kuwa aliwasaidia Wamarekani kumuua kiongozi wa kundi hilo Ahmed Godane.
Mwingine aliyepigwa risasi anadaiwa kuwa alisaidia Wamarekani kumuua Adnan Garaar, anayeaminika kuongoza shambulio la kigaidi katika duka la Westgate nchini Kenya mwaka wa 2013.
-BBC

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA