PPFT : GWAJIMA AFUTIWE USAJILI KWA KUTOA KAULI ZA UCHOCHEZI
Mwenyekiti wa ushirika wa wachungaji hao Askofu Pius Ikongo mwenye makao yake katika Halmashauri ya wilaya ya Mwanga amesema,kauli hizo zinaweza kubadili fikra za wananchi na kuzaa chuki dhidi ya serikali yao na kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani.
Askofu Ikongo ametoa tamko hilo katika taarifa yake kwa vyombo vya habari na kueleza kuwa kitendo kilichofanywa na Askofu Gwajima kinapaswa kulaaniwa na wapenda amani wote waliopo ndani na nje ya nchi.
Mwenyekiti huyo wa ppft amesema, kosa kubwa ambalo limewaumiza wachungaji wa Kipentekoste ni kitendo cha Askofu Gwajima kutumia Kanisa kama jukwaa la kisiasa kwa kuleta uchonganishi kati ya serikali ya awamu ya nne na iliyopo madarakani.
0 comments:
Post a Comment