RAIS WA PHILIPPINES AWATAKA WANANCHI KUWAUWA KWA KUWAPIGA RISASI WAFANYABIASHARA WA DAWA ZA KULEVYA
Rais mteule wa Philippines, Rodrigo Duterte, amewahamasisha wananchi wa nchi hiyo kuwapiga risasi na kuwauwa wafanyabiashara wa dawa za kulevya na kukabiliana nao katika makazi yao.
Katika hotuba yake kwa njia ya televisheni jana rais huyo amewasihi wananchi kusaidia vita dhidi ya uhalifu, na ameahidi kuwapatia zawadi wale wote watakaoshiriki vita hiyo.
Kauli hiyo ya rais Duterte imeonekana kuungwa mkono na Meya moja ambaye ameipatia polisi zaidi ya paundi 2,000 kwa kuwauwa wasafirishaji dawa za kulevya.
Rais mteule wa Philippines Rodrigo Duterte kati kati akipiga Selfie
0 comments:
Post a Comment