Wednesday 29 June 2016

RC MAKONDA ATEMBELEA BANDA LA UN KATIKA VIWANJA VYA SABASABA

Katika kuelekea kilele cha Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ametembelea banda la Umoja wa Mataifa (UN) lililopo katika ukumbi wa Karume kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar.

Makonda alifika katika banda hilo na kupata nafasi ya kupata maelezo kutoka kwa wafanyakazi wa UN kuhusu kazi ambazo zinafanywa na shirika hilo hapa nchini.

24a7d672-88a7-4024-bc72-99911346b847
Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu (kulia) akitoa maelezo ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (katikati) alipotembea banda la shirika hilo lililopo katika ukumbi wa Karume kwenye Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar.
26665f2e-d3e0-448a-abf9-abd978f2904b
168168bf-4b6a-4701-ae35-625c9dd42c26
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu kuhusu Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambayo yanatakiwa kumfikia kila mwananchi alipotembelea banda la Umoja wa Mataifa lillilopo katika ukumbi wa Karume kwenye Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar.
a53dc2a5-b305-41ad-869c-efdc98bf24ec
168168bf-4b6a-4701-ae35-625c9dd42c26
48536637-39a1-49d1-84e0-d5991f06f696
Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu akimwonyesha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) yaliyobandikwa katika banda la UN na jinsi walivyojipanga katika kuelimisha wananchi kuhusiana na malengo hayo kwenye Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar.
a6b8ce8b-3e3c-447d-956c-eaa90837fa7c
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akisaini kitabu cha wageni katika banda la Shirika la Umoja wa Mataifa lililopo katika ukumbi wa Karume kwenye Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar. Kulia ni Maafisa Habari wa Umoja wa Mataifa, Hoyce Temu na Usia Nkhoma Ledama. RC Makonda amekuwa mgeni kwanza mashuhuri kutembelea banda hilo na kutoa baraka zake kwenye maonyesho hayo.
cae027d5-302e-4ef0-b32b-7605a85de394
4596858e-e78b-45f1-abad-1abc1fd4a452
Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu katika picha ya pamoja huku wakiwa na bango maalum linalowakilisha rangi za malengo 17 ya SDGs na mmoja wa vijana aliyetembelea banda la Umoja wa Mataifa lililopo kwenye ukumbi wa Karume kwenye maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar.
6d8cdd26-c801-41ac-b080-5a6e4f3ec817
Afisa Habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama akizungumza na waandishi wa habari kwa lengo la kuhamasisha wananchi kutembelea banda hilo na kujifunza Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu SDGs na kujua shughuli mbalimbali zinazofanywa na Shirika hilo hapa nchini.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA