TANZIA:: COMEDIAN KUNDAMBANDA AFARIKI DUNIA
Taarifa za awali
zinaeleza kuwa msanii wa vichekesho Ismail Issa Makombe maarufu
zaidi kama KUNDANBANDA amefariki dunia nyumbani kwao Masasi mkoani Mtwara huku.
Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu Kundambanda amefariki alfajiri ya leo mjini Masasi.Alikuwa shambani kwake takribani mwezi mmoja uliopita akiendelea na shughuli za kilimo cha ufuta, wiki iliyopita alirudi Masasi kuendelea na shughuli zake zingine, ndipo majuzi alibanwa na kifua akaenda mwenyewe hospitali huku akiendesha gari yeye mwenyewe akapatiwa matibabu na jana kuanzia mchana ndipo hali ilipobadilika na hatimaye leo alfajiri kufariki dunia.
Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu Kundambanda amefariki alfajiri ya leo mjini Masasi.Alikuwa shambani kwake takribani mwezi mmoja uliopita akiendelea na shughuli za kilimo cha ufuta, wiki iliyopita alirudi Masasi kuendelea na shughuli zake zingine, ndipo majuzi alibanwa na kifua akaenda mwenyewe hospitali huku akiendesha gari yeye mwenyewe akapatiwa matibabu na jana kuanzia mchana ndipo hali ilipobadilika na hatimaye leo alfajiri kufariki dunia.
Kundambanda alijipatia
umaarufu kupitia kundi la vituko show ambapo zaidi alikuwa akiigiza kama askari
wa kitengo cha barabarani "Trafiki" na kutumia lafudhi ya watu wa
Mtwara. Sambamba na hilo Kundambanda katika kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka
jana alikuwa gumzo hasa pale alipojitokeza na kuwa mgombea ubunge jimbo la Masasi kupitia tiketi ya
CUF na kuleta hali ya sintofahamu ndani ya UKAWA hasa ambapo Dr.
Makaidi aliesimamishwa kupitia NLD ndiye aliyekuwa mgombea rasmi kupitia umoja
huo kabla mauti hayajamkuta zikiwa zimebakia siku chache kufikia kilele cha
kampeni.
Lakini hata hivyo katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Disemba 2015 baada ya ule wa Oktoba kutofanyika kutokana na kifo cha aliyekuwa mgombea wa awali wa UKAWA, Mhe. Emmanuel Makaidi (NLD) Kundambanda alipata kura 14,069 dhidi ya kura 16,597 za (mshindi) Rashid Chua Chua kutoka CCM.
Lakini hata hivyo katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Disemba 2015 baada ya ule wa Oktoba kutofanyika kutokana na kifo cha aliyekuwa mgombea wa awali wa UKAWA, Mhe. Emmanuel Makaidi (NLD) Kundambanda alipata kura 14,069 dhidi ya kura 16,597 za (mshindi) Rashid Chua Chua kutoka CCM.
![]() |
Kundambanda akiwa jukwaani wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu 2015 |
Kifo cha Kundambanda kimekuwa pigo jingine kwa kundi la VITUKO SHOW hasa likiwa limempoteza aliyekuwa mchekeshaji wa kipekee Mohammed Abdallah maarufu "KINYAMBE".
Tayari baadhi ya wasanii wameonesha kuguswa na msiba huu na kuanza kuweka post katika mitandao ya kijamii.
Nimekuwekea moja kati ya kazi alizofanya katika kundi la vituko Show
0 comments:
Post a Comment