Tuesday 4 October 2016

WATANZANIA WATAKIWA KUJENGA MOYO WA KUJITOLEA


  Mmoja wa wanakikundicha Marafiki wa Batuli aliyejulikana kwa jina la Tausi Swalehe akiwa anakabidhi anagawa peniseli kwa baadhi ya wanafunzi ambao ni yatima wanaosoma katika shule ya msingi Ngarenaro ilipo katika kata ya Sokoni one ndani ya jiji la Arusha
  Wanakikundi wa kikundi cha marafiki wa batuli wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi waliowagawia msaada wa sare za shule ,penseli ,madaftari na kalamu ikiwa ni moja ya mchango wao kama wao wanakikundi .
                                                                                                Na Woinde Shizza Arusha
 
Wazazi na watanzania wameaswa kujenga moyo Wa kujitolea kwa makundi maalumu yasiojiweza nakuwapa kile mungu alichowajaalia nakuondoa ubaguzi kwa watoto yatima waliochiwa na ndugu zao. 

Hayo yalisemwa na Tausi swalehe baada ya kikundi cha marafiki Wa batuli kufika kutoa msaada kwenye shule za unga ltd,na Sahel zilizopo kata ya Sokon 1 jijini Arusha nakuwata jamii kuwa na moyo huo wa kusaidia yatima na makundi yasiojiweza. 

Alisema kuwa msaada waliotoa unathamani ya tsh.700,000 vikiwemo madaftari'sare za shule,penseli na pen ambazo zitawapunguzia adha watoto wenye uhitaji wakiwemo yatima na wasiojiweza ambao wameshindwa kujihudumia na kufikia malengo. 

Alisema kuwa ni vizuri kwa jamii kuendelea kuzijali familia zisizojiweza na mayatima iliwaweze kufikia malengo yao yakupata elimu itayowasaidia kujikwamua kimaisha na kuondokana na utegemezi. 
 
''Sio wote wenye kuweza kujiendesha kimaisha yatupasa kama jamii kujipanga nakuweza kuwasaidia wenye uhitaji natusingoje kuiachia serikali pekee''alisema Tausi. 

Akipokea msaada huo kwa niaba ya wanafunzi hao wenye uhitaji mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Unga Ltd Rachel Mussa alisema kuwa wapo wengi katika jamii wenye fedha lakini wamekuwa hawatumii vipato vyao katika kusaidia makundi yenye uhitaji. 

Akatoa rai kwa makampuni na wenye kuguswa kuweza kujitolea kwa kile kidogo mungu alichowajaalia kwani wapo watoto wenye uhitaji nao wajitokeza kuwasaidia. 
 
Nae Mwanafunzi mwenye uhitaji kwa niaba ya wenzake 86 Konsolata Michael alisema kuwa wanashukuru sana kwa msaada huo kwani umukuja wakati muufaka na kuwataka kuendelea kusaidia watoto yatima na wasiojiweza na mungu awazidishie pale mlipopunguza kwa ajili yetu.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA