Tuesday 8 November 2016

HOSPITALI YA MUHIMBILI YAPOKEA MSAADA WA MASHINE YA UTRASOUND YENYE UWEZO MKUBWA WA KUNG’AMUA MAGONJWA YA FIGO

Hospitali ya Taifa Muhimbili imepokea  msaada wa mashine kubwa na ya kisasa  ya Utra Sound maalum  kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa wenye matatizo ya Figo.

Msaada huo umetolewa  jana na Hospitali ya Chuo Kikuu cha Haukeland cha nchini Norway ambapo pamoja na mambo mengine wameahidi kuendelea kutoa ushirikiano  katika maeneo ya elimu , utafiti pamoja na vifaa tiba.

Daktari Bingwa wa magonjwa ya Figo ambaye pia Mhadhiri kutoka MUHAS Paschal Ruggajo  amesema mashine hiyo itasaidia kuchukua sampuli ya figo kwa ajili ya kugundua  magonjwa  ya Figo , kuweka vifaa kwenye mishipa damu kwa wagonjwa wanaoanzishiwa matibabu ya uchujaji wa damu na kugundua matatizo mbalimbali ya Figo.

“ Kwa muda mrefu sasa tumekua na ushirikiano wa karibu kati ya Hospitali hiyo , MUHAS na MNH  na wametusaidia kufundisha Madaktari sita wa Figo , wameshatoa mashine za kusafisha Figo na sasa wametupatia mashine hii kubwa ya Utra Sound kwakweli tunawashukuru kwa msaada wao.” Amesema Dk. Ruggajo.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili , Dk . Hedwiga Swai ambaye ni Mkurugenzi wa Huduma za Tiba ameishukuru Hospitali hiyo ya Haukeland  na kusisitiza kuwa msaada huo umekuja wakati muafaka kwakua  mashine hiyo itasaidia sana katika kitengo cha Figo
Profesa Einar Svastard ( kulia)   akimkabidhi  msaada wa mashine kubwa ya kisasa ya Utrasound  Mkurugenzi wa huduma za tiba  MNH Dk. Hedwiga Swai  .
Profesa Einar Svastard akimfanyia uchunguzi mgonjwa kwa kutumia mashine hiyo

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA