Sunday 20 November 2016

WANANCHI INDIA WAJITOLEA KUMCHANGIA FIGO WAZIRI WAO

Wananchi wengi wa India wamejitolea kumchangia figo Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Bi. Sushma Swaraj baada ya kutwitti anafanyiwa vipimo vya kupandikiziwa figo.

Bi. Swaraj mwenye umri wa miaka 64, amekuwa na historia ya kuugua kisukari na alikuwa amelazwa kwenye hospitali huko Delhi, mapema mwaka huu.

Bi. Swaraj ni mmoja wa mawaziri wenye uzoefu wa juu katika serikali ya Waziri Mkuu wa India Narendra Modi.

Siku ya jumanne, Swaraj alitwitti kuwa anafanyiwa tiba inayojulikana kitaalam kama dialysis baada ya figo yake kushindwa kufanyakazi.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA