Sunday 8 January 2017

I-LEARN EAST AFRICA LTD YAKABIDHI ZAWADI KWA WASHINDI WA JINSHINDIE T-SHIRT

Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo I-Learn East Africa Ltd Bw. Deus Ntukamazina akimkabidhi zawadi ya T-shirt mshindi wa kwanza Bi Fortunate Kayuni katika ofisi za I-Learn Mikocheni jijini Dar Es Salaam

Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo I-Learn East Africa Ltd Bw. Deus Ntukamazina akimkabidhi zawadi ya T-shirt mshindi pili Bw.Sadick Omary katika ofisi za I-Learn Mikocheni jijini Dar Es Salaam

Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo I-Learn East Africa Ltd Bw. Deus Ntukamazina akimkabidhi cheti mshindi wa kwanza Bi Fortunate Kayuni



Kampuni ya I-Learn East Africa Ltd inayojihusisha na huduma ya kutoa na kuendesha mafunzo kwa makampuni, taasisi pamoja na watu binafsi imekabidhi zawadi kwa washindi wawili katika shindano la Jishindie T-shirt na I-Learn ambapo vigezo vilikuwa ni kushiriki kwa kusoma na kujibu maswali katika tovuti ya I-learn kisha kufikisha alama 70 na zaidi.


Zawadi hizo zilikabidhiwa na Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo I-Learn East Africa Ltd Bw. Deus Ntukamazina ambapo mshindi wa kwanza Bi Fortunate Kayuni alipata alama zaidi ya 80 na mshindi wa pili Bw.Sadick Omary ambaye alipata zaidi ya alama 70 katika ofisi za I-Learn Mikocheni jijini Dar Es Salaam.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA