BREAKING::MASHAMBULIZI MENGINE YATOKEA LAMU
12:08 |
No Comments |
Mashambulizi yalitokea mara ya kwanza katika eneo la Mpeketoni ambapo zaidi ya watu 60 waliuawa
Watu waliojihami wamevamia kijiji cha Pandanguo katika Kaunti ya Lamu Pwani ya Kenya.
Chifu wa eneo hilo Karisa Charo Karisa, anasema kuwa shule na nyumba nne ziliteketezwa katika mashambulizi hayo yaliyofanywa usiku wa kuamkia leo.
Kwa sasa hakuna taarifa zozote kuhusu majeruhi wa mashambulizi hayo.Duru zinaarifu kuwa washambuliaji hao waliiba bunduki kutoka kwa watu polisi wa dharura na kufanya mashambulizi hayo.
Duru zinasema kuwa washambuliaji hao waliiba bunduki sita kutoka kwa polisi wa dharura kabla ya kuteketeza nyumba.
Kwa sasa hakuna taarifa zozote kuhusu majeruhi.
Inaarifiwa kuwa wanajeshi wamepelekwa katika eneo hilo kudhibiti usalama.
Mnamo mwezi Juni watu watano waliuawa katika eneo hilo la Pandanguo ambalo liko umbali wa kilomita 30 kutoka Mpeketoni ambako mashambulizi mengine yaliwaacha watu zaidi ya sitini wakiwa wameuawa.
Waathiriwa wengi wa mauaji walipatwa wakiwa wamefungwa mikono nyuma ya migongo na koo zao zikiwa zimekatwa.
Eneo la Lamu ambao liko Pwani ya Kenya limekuwa na mashambulizi ya mara kwa mara tangu mwezi Juni huku watu wakiuawa kwa misingi ambayo bado ni tata.
Mashambulizi ya Kwanza yaliyofanyika mjini Mpeketoni, yalisemekana kufanywa na kundi la wanamgambo la Al Shabaab ingawa serikali alilalaumu wanasiasa kuyachochea mashambulizi hayo.
NA BBC
NA BBC
Related Posts:
JESHI LAPINDUA NCHI THAILAND Mkuu wa majeshi nchini Thailand ametangaza mapinduzi , akisema jeshi sasa linachukua udhibiti wa serikali.Katika taarifa iliyotolewa kupitia kw… Read More
Waziri wa Usalama wa taifa wa Somalia ajiuzulu Waziri wa Usalama wa Taifa wa Somalia amejiuzulu. Abdikarim Hussein Guled amejiuzulu baada ya kujiri shambulio la kigaidi karibu na bu… Read More
26 wauawa katika shambulizi Borno,Nigeria Mashambulizi yaliyofanywa awali na Boko Haram katika mji wa Jos Kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Boko Haram wametuhumiwa kwa kuwaua watu … Read More
CHATU ALIYEKUWA ANATISHIA MAISHA YA WANAINCHI MBEYA AKAMATWA Hii ni Video ikionesha namna ambavyo Chatu aliweza kukamatwa.. T… Read More
MATOKEO YA UCHANGUZI MALAWI YATANGAZWA. Hatimaye Tume ya uchaguzi nchini Malawi imeanza kutoa matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo jumanne iliyopita. Ma… Read More
0 comments:
Post a Comment