ANTI LULU: NATAKA KUZAA NA DIAMOND
09:12 |
No Comments |
Msichana wa mjini asiyeishiwa matukio Bongo, Lulu Mathias Semagongo ‘Anti Lulu’ amefunguka kwamba yupo tayari kuzaa na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kwani amepata taarifa kwamba anasaka mtoto lakini wanawake anaokuwa nao hawataki kumzalia, Ijumaa Wikienda linakupasha.
BILA KUMUNG’UNYA MANENO
Akizungumza na gazeti hili bora la mastaa Bongo akiwa dukani kwake Kinondoni jijini Dar, wikiendi iliyopita, Anti Lulu bila kumung’unya maneno, alifunguka kwamba hivi karibuni alifuatwa na ndugu wa karibu wa Diamond au Dangote kama anavyopenda kujiita na kumuomba afanye jitihada azae naye.
MAKUBWA!
Alidai aliambiwa kuwa kila Diamond akimpa kibendi mwanamke, huwa mwanamke huyo anakwenda kukitoa bila hata ridhaa yake (Diamond).
“Ndugu wa Diamond alinifuata hapa dukani kwangu akanitaka nizae na Dangote kwani anasaka sana mtoto na kila akimpa mwanamke mimba huwa anaichoropoa bila kuafikiana naye.“Sababu kubwa ya wanawake hao kutoa mimba ni kutokana na mpenzi wa Diamond ambaye ni Wema (Isaac Sepetu) kudaiwa kuloga ili mwanamke yeyote asizae naye na kila akimpa mimba mwanamke inatoka au anakwenda kutoa mwenyewe bila sababu yoyote,” alisema Anti Lulu.
Pamoja na tetesi hizo, Anti Lulu alisema haogopi lolote kwani amejizatiti ndiyo maana amejitokeza hadharani na kutaka kuzaa na Diamond.
Anti Lulu alisema kwamba anaamini Diamond atamkubali japokuwa hawajawahi kuzungumzia hiyo ishu wakiwa pamoja na kwamba walishakutana na kuzungumza mambo mengine.
“Nataka na nimejizatiti vilivyo kwa ajili ya kumzalia Diamond ‘kabebi’ kazuriii...
“Nataka nione hiyo kulogwa inakuwaje hao wanaotoaga mimba zake bila sababu?
MTOTO MZURI
“Naamini mimi nitamzalia mtoto mzuri kabisa kwani nimejipanga tayari na siogopi kitu chochote.
“Diamond hajawahi kunitongoza ila kuna siku moja tulionana maeneo ya Kinondoni halafu nikaja kuambiwa na mmoja wa marafiki zake kwamba aliponiona siku hiyo alinisifia.
“Niliambiwa alisema kwamba mimi ni mwanamke mzuri na umbo langu ni zuri hivyo naomba akubali tu nimzalie jamani,” alisema Anti Lulu ambaye aliwahi kuwa prizenta wa runinga na mwigizaji wa sinema za Kibongo.
BIFU?
Anti Lulu alidai kwamba japokuwa anaamini kabisa kwamba Wema atakasirika, hatajali kama mbwai iwe mbwai na yupo tayari kuanzisha naye bifu zito.
Alisema kila mmoja atakuwa na nafasi yake kwa Diamond na kwamba kikubwa anataka kuzaa na Diamond halafu amkabidhi mtoto kila mmoja aendelee na maisha yake.
NENO!
“Najua Wema atakuwa na bifu na mimi lakini sijali kwa sababu nimeamua na yeye ni mpenzi wa Diamond tu siyo mke wake kwani hawajafunga ndoa.
“Angekuwa ni mkewe ndiyo ningeogopa lakini hivihivi sihofii chochote,” alisema Anti Lulu.
DIAMOND, WEMA NA PENNY
Diamond aliwahi kuripotiwa kumpa ujauzito aliyekuwa mpenzi wake, Penniel Mungilwa ‘Penny’ lakini baada ya muda mfupi ilidaiwa kuchoropoka.Pia aliwahi kudaiwa kumpachika kibendi Wema ambaye naye ilidaiwa ilichoropoka.
Kwa upande wake Anti Lulu aliwahi kutoka na wanaume kadhaa wakiwemo Bond Bin Sinan na Amani ambao hakufanikiwa kuwazalia watoto.
SWALI LENYE HOJA!
Baadhi ya watu waliomsikia Anti Lulu akitangaza ishu hiyo walijiuliza swali moja tu: ‘Hivi kweli Anti Lulu huyuhuyu anaweza kuwa mama bora?’Diamond hakupatikana ili kufikishiwa ujumbe huo na kujua namna alivyopokea taarifa hiyo ya Anti Lulu.
Akizungumza na gazeti hili bora la mastaa Bongo akiwa dukani kwake Kinondoni jijini Dar, wikiendi iliyopita, Anti Lulu bila kumung’unya maneno, alifunguka kwamba hivi karibuni alifuatwa na ndugu wa karibu wa Diamond au Dangote kama anavyopenda kujiita na kumuomba afanye jitihada azae naye.
MAKUBWA!
Alidai aliambiwa kuwa kila Diamond akimpa kibendi mwanamke, huwa mwanamke huyo anakwenda kukitoa bila hata ridhaa yake (Diamond).
“Ndugu wa Diamond alinifuata hapa dukani kwangu akanitaka nizae na Dangote kwani anasaka sana mtoto na kila akimpa mwanamke mimba huwa anaichoropoa bila kuafikiana naye.“Sababu kubwa ya wanawake hao kutoa mimba ni kutokana na mpenzi wa Diamond ambaye ni Wema (Isaac Sepetu) kudaiwa kuloga ili mwanamke yeyote asizae naye na kila akimpa mimba mwanamke inatoka au anakwenda kutoa mwenyewe bila sababu yoyote,” alisema Anti Lulu.
Pamoja na tetesi hizo, Anti Lulu alisema haogopi lolote kwani amejizatiti ndiyo maana amejitokeza hadharani na kutaka kuzaa na Diamond.
Mkali wa Bongo Fleva 'Diamond Platinum' akiwa na mpenzi wake wema Sepetu.
IMANIAnti Lulu alisema kwamba anaamini Diamond atamkubali japokuwa hawajawahi kuzungumzia hiyo ishu wakiwa pamoja na kwamba walishakutana na kuzungumza mambo mengine.
“Nataka na nimejizatiti vilivyo kwa ajili ya kumzalia Diamond ‘kabebi’ kazuriii...
“Nataka nione hiyo kulogwa inakuwaje hao wanaotoaga mimba zake bila sababu?
MTOTO MZURI
“Naamini mimi nitamzalia mtoto mzuri kabisa kwani nimejipanga tayari na siogopi kitu chochote.
“Diamond hajawahi kunitongoza ila kuna siku moja tulionana maeneo ya Kinondoni halafu nikaja kuambiwa na mmoja wa marafiki zake kwamba aliponiona siku hiyo alinisifia.
“Niliambiwa alisema kwamba mimi ni mwanamke mzuri na umbo langu ni zuri hivyo naomba akubali tu nimzalie jamani,” alisema Anti Lulu ambaye aliwahi kuwa prizenta wa runinga na mwigizaji wa sinema za Kibongo.
BIFU?
Anti Lulu alidai kwamba japokuwa anaamini kabisa kwamba Wema atakasirika, hatajali kama mbwai iwe mbwai na yupo tayari kuanzisha naye bifu zito.
Alisema kila mmoja atakuwa na nafasi yake kwa Diamond na kwamba kikubwa anataka kuzaa na Diamond halafu amkabidhi mtoto kila mmoja aendelee na maisha yake.
NENO!
“Najua Wema atakuwa na bifu na mimi lakini sijali kwa sababu nimeamua na yeye ni mpenzi wa Diamond tu siyo mke wake kwani hawajafunga ndoa.
“Angekuwa ni mkewe ndiyo ningeogopa lakini hivihivi sihofii chochote,” alisema Anti Lulu.
DIAMOND, WEMA NA PENNY
Diamond aliwahi kuripotiwa kumpa ujauzito aliyekuwa mpenzi wake, Penniel Mungilwa ‘Penny’ lakini baada ya muda mfupi ilidaiwa kuchoropoka.Pia aliwahi kudaiwa kumpachika kibendi Wema ambaye naye ilidaiwa ilichoropoka.
Kwa upande wake Anti Lulu aliwahi kutoka na wanaume kadhaa wakiwemo Bond Bin Sinan na Amani ambao hakufanikiwa kuwazalia watoto.
SWALI LENYE HOJA!
Baadhi ya watu waliomsikia Anti Lulu akitangaza ishu hiyo walijiuliza swali moja tu: ‘Hivi kweli Anti Lulu huyuhuyu anaweza kuwa mama bora?’Diamond hakupatikana ili kufikishiwa ujumbe huo na kujua namna alivyopokea taarifa hiyo ya Anti Lulu.
Read more: http://www.vitukovyamtaani.com/2014/09/anti-lulu-nataka-kuzaa-na-diamond.html#ixzz3Cha8SPju
Related Posts:
KIPINDI CHA UNYAYO WANGU: DAVID MANOTI AZUNGUMZIA ADHABU YA WABUNGE WA UPINZANI BUNGENI Unyayo wangu ni kipindi kipya kabisa kinachokujia kupita Tone Tv, ambacho kinaletwa kwenu na Mtangazaji wetu Eddie Nyota , kinacholenga s… Read More
DC KIHATO: NI AIBU MWANAMKE KUTOKA ALFAJIRI KUTAFUTA KUNI, MUME AMELALA! Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Luteni mstaafu Abdallah Kihato, akipanda mti katika Ofisi ya Kijiji cha Magoza kama sehemu ya utunzaji wa mazingir… Read More
CHADEMA WAMTAKA RAIS MAGUFULI AMFUATE LOWASSA ILI AMSHAURI KUHUSU SUKARI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemtaka Rais John Magufuli kuweka siasa kando na kuomba ushauri kwa waziri mkuu wa zamani, Edward L… Read More
KAMA UMEPANGA NYUMBA AU KUPANGISHA TAARIFA HII IKUFIKIE KUTOKA JESHI LA POLISI DAR ES SALAAM JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewataka wenyeviti wa serikali za mitaa kushirikiana na wenye nyumba kuhakikisha wapangaji katika n… Read More
BEN POL NA CHEGE WATEMBELEA WATOTO WENYE MATATIZO YA KUPINDA MIGUU KATIKA HOSPITAL YA CCBRT Wasanii wa muziki wa kizazi kipya, ‘Chege Chigunda’ na Ben Pol wakishuhudia Daktari wa Watoto, Prosper Alute akimhudumia mtoto mwenye umri wa mwezi … Read More
0 comments:
Post a Comment