Saturday 20 December 2014

KOCHA CRYSTAL PALACE AFUTWA KAZI


Neil Warnock amekuwa meneja wa kwanza wa ligi ya Uingereza kupigwa kalamu msimu huu baada ya kufutwa kazi na Crystal Palace.
Mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 66 alijiunga na timu hiyo kwa mara ya pili mnamo mwezi Agosti mwaka 2014 kufuatia kuondoka kwa Tony Pulis.
Hatua hiyo inafutia kichapo cha mabao 3-1 nyumbani dhidi ya Southampton siku ya boxing dei.
Palace kwa sasa iko katika eneo la kushushwa daraja ikiwa na alama moja juu ya Hull City ilioko katika nafasi ya 17.
Meneja msaidizi Keith Millen sasa atachukua fursa ya kuiongoza kilabu hiyo dhidi ya QPR siku ya jumapili.
Warnock alishinda michuano mitatu pekee kati ya mechi 16 alizosimamia.
-BBC

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA