Tuesday 30 December 2014

TAARIFA KUHUSU: NDEGE YA AIRASIA QZ8501 ILIYOPOTEA NA WATU 162



Kikosi cha wanamaji nchini Indonesia kikisali kabla ya kuanza zoezi la kuitafuta Ndege ya AirAsia QZ8501 katika bandari ya Pangkal Pinang kwenye kisiwa cha Sumatra.
Kikosi cha wanamaji kikiwa kazini kuitafuta ndege iliyopotea.
Ndugu wa watu waliokuwa kwenye ndege iliyopotea wakifarijiana huku wengine wakilia kwa uchungu.
ZOEZI la kuitafuta Ndege ya AirAsia QZ8501 iliyopotea ikiwa na watu 162 ikitokea Indonesia kwenda Singapore jana limeendelea leo asubuhi.
Taarifa zilizopatikana kutoka eneo la utafutaji ndege hiyo zinadai kwamba mabaki ya AirAsia QZ8501 yameonekana baharini na kuna uwezekano ndege hiyo ipo chini ya bahari.
Saa 11:36 asubuhi, Ndege y

a AirAsia QZ8501 iliondoka Indonesia.
Saa 12:12 asubuhi rubani aliomba kuipandisha ndege mpaka futi 38,000 kutokana na hali mbaya ya hewa.
Saa 12:16 asubuhi AirAsia ilikuwa bado inaonekana kwenye rada.
Saa 12:18 asubuhi AirAsia QZ8501 ikapoteza mawasiliano na rada na mpaka sasa bado haijapatikana.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA