Wednesday 28 January 2015

"NILIACHA KAZI ILI KUFUATA KIPAJI CHANGU " MC PILI PILI AFUNGUKA



Alizaliwa tarehe 1 Oktoba 1985 wengi wanamfahamu zaidi kama Mc Pili Pili lakini jina lake halisi ni Emanuel Mathias mchekeshaji na mshereheshaji anayefanya vizuri katika tansia ya komedi nchini Tanzania.
Katika mahojiano maalum na Funguka Live Blog Mc pili pili alieleza kuwa aliamua kufanya maamuzi magumu ya kuachana taaluma yake ya ualimu alipokuwa akifundisha shule ya Dct Jubilee High School mjini Dodoma na kuelekea jijini Dar es salaam…. “Nilikuwa mwalimu wa sekondari kwa miaka sita (6) nikaamua kuacha na kuhama toka Dodoma kuja Dar es salaam,niliamua kufuata kipaji changu”
Mc pili pili akifanya mambo katika moja ya show zake
“Kwa muda wa miaka kumi na tano nimekuwa mshereheshaji na mchekeshaji ila katika miaka mitano ya karibuni ndio nimekuwa serious kwenye komedi”.Pili pili aliongeza kwa kuwataja wale waliomuhamasisha na kumpa ari ya kuanza kufanya komedy kama kazi, “kwa hapa nyumbani naweza kusema ni Joti,Masanja pamoja na marehemu Sharo millionea lakini kwa Afrika mashariki ni Eric Omondi na Afrika kwa ujumla siwezi kuacha kuwataja Basket Mouth na Trevoh Noah ila nje ya Afrika Kevin Hart amekuwa role model wangu”…
Mc pili pili akiwa na Joti
Mc pili pili ambaye pia ni mtangazaji wa redio Times Fm na mkurugenzi wa Pili pili events alikiri kuwa kwa sasa aina ya komedi anayofanya “stand up comedy” ile ya kwenye majukwaa bado haijapata muitikio mkubwa hapa nchini kama ilivyo kwa majirani zetu wa Kenya na Uganda. “Kikubwa ni kuitambulisha zaidi na zaidi  nitapeform Dar es salaam,Arusha ,Dodoma na Mwanza mwaka huu  ila pia nina mpango wa kuperform  nchini Marekani na U.K kwa Watanzania waishio huko nadhani kwa nguvu hii “stand up comedy” itapata kukubalika zaidi na zaidi”.

Funguka live Blog ilipotaka kujua kama Mc pili pili anampango wa kufanya falimu alisema kuwa kwa sasa bado hajaamua ila baadae anaweza akaingia katika kucheza filamu kwa sasa naweka videos za kazi yangu Youtube na kwa kweli zinafanya vizuri.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA