Thursday 15 January 2015

WATANZANIA WATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA KWA FAIDA YAO

Image result for faida za kutunza mazingira 
WAKATI mvua zikiendelea kunyesha ndani na nje ya jiji la Dar es salaam, Watanzania wametakiwa kutunza mazingira yanayowazunguka ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko yanayoweza kuhatarisha maisha yao.
 
Akizungumza na Funguka live blog  jijini jana, Mwenyekiti wa mtaa wa Kigogo darajani, Bakari Nnyange, alisema  kuwa kijiografia wakazi wengi bado hawana elimu kuhusu  utunzaji wa mazingira katika kipindi hiki.

 
Aliwataka wananchi kuwa makini na utupaji taka hovyo kwani imebainika kuwa ni chimbuko la magonjwa hatarishi hasa kwa watoto ambao wanaishi na kulelewa kwenye mazingira yasiyo salama.
 
“Kuna haja ya wananchi wenyewe kuangalia njia ya kuepukana na magonjwa ya mlipuko, sio kila kitu mnasubiri kufanyiwa na serikali, usafi ni jukumu la kila mtu, na usafi wa mtu uanzia nyumbani kwake” alisema Nnyange.
 
Naibu  Meya wa Manispaa ya Ilala, Kheri Kessy alisema asilimia 70 ya makazi  ya wananchi wa Dar  es Salaam, yamejengwa kiholela.
 
Aliongeza kuwa kutokana na jiografia hiyo asilimia 30 tu  ya makazi  ndiyo yaliyojengwa katika mfumo rasmi, jambo ambalo linailazimu serikali kwa sasa na baadaye kutumia kiasi kikubwa cha fedha cha kutafuta  eneo mbadala kwa ajili ya wananchi wake.
 
“Mwito wangu kwa taasisi za serikali na  binafsi kutumia kila fursa zinayopatikana , katika  kubadili maisha ya Watanzania, pia  wananchi  waelewe kuwa  serikali ina changamoto kubwa ya kukabiliana na tatizo hilo” alisema Kessy.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA