WENGER, FERDINAND, WAMSHAMBULIA DIEGO COSTA
Wenger amemponda mwamuzi Mike Dean kwa kile alichosema alimuogopa Diego Costa ambaye alistahili kupewa kadi nyekundu baada ya kumchezea vibaya mlinzi mwingine wa Arsenal Laurent Koscienly lakini Mike Dean akaishia kumpa kadi ya njano.
Alan Shearer amemlaumu Paulista kwa kuingia katika mtego wa tabia za Diego Costa na kusababisha kutolewa nje kwa kadi nyekundu. Katika mechi hiyo ambayo Arsenal walifungwa mabao 2-0 iliisha kwa Arsenal kuwa pungufu ya wachezaji wawili mara baada ya Saint Carzola nae kuoneshwa kadi nyekundu.
Watu wengi nchini England wanataka kuona FA ikichukua hatua dhidi ya Diego Costa ikiwa ni pamoja na kumfungia sanjari na faini kwa tabia zake za kuwatupia makonde wapinzani pamoja na mchezo wake usio wa kistaarabu.
0 comments:
Post a Comment