Thursday 1 October 2015

MADRID NAYO YATAKATA,MANCHESTER UNITED IKIPATA USHINDI WA KWANZA UEFA,





Vinara wa Ligi Kuu ya Uingereza Manchester United wamepata ushindi wao wa kwanza katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya katika hatua ya makundi baada ya kutoka nyuma na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya VfL Wolfsburg.



Wakati Chelsea pamoja na Arsenal zikiwa zimepoteza michezo yao jumanne, United walikuwa katika hatari ya kufuata nyayo zao baada ya Daniel Caligiuri kufunga bao lililozaliwa kutokana na pasi sita.



Hata hivyo Juan Mata aliisawazishia Manchester United kwa mkwaju wa penati uliotokana baada ya kumnawisha mpira beki wa Wolfsburg, na kisha Chris Smalling akiunganisha pande la nyuma la Mata na kuandika bao la pili.

  Wayne Rooney na Anthony Martial wakianzisha mpira baada ya kufungwa bao la kwanza
                      Chris Smalling akipachika wavuni bao la pili la Manchester United
Nyota Cristiano Ronaldo ameifikia rekodi ya Raul ya kuifungia Real Madrid kwa kuifungia magoli mengi na kufikisha idadi ya kupachika magoli 500 kwa kufunga mabao mawili dhodi ya Malmo nchini Swedeni.


Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Ureno aliandika bao la kwanza katika mchezo huo wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya wa kundi A, kwa kuunganisha pande alilopewa na Isco na kisha baadae kupachika tena bao la pili.

Matokeo mengine ni Borussia Mönchengladbach 1 - 2 Man City, Shakt Donsk 0 - 3 Paris St G, CSKA 3 - 2 PSV, FC Astana 2 - 2 Galatasaray pamoja na Atl Madrid 1 - 2 Benfica.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA