Thursday 12 May 2016

COMEDIAN KINYAMBE AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji aliyekuwa anakuja juu kwa kasi Mohammed Abdallah  "KINYAMBE" amefariki dunia leo usiku huko nyumbani kwao Mbeya.

 Mmoja wa wanandugu wa Kinyambe amethibitisha  kuwa msanii huyo wa filamu  ambaye pia alikuwa akijulikana kwa jina la James, amefariki baada ya kuugua kwa siku kadhaa.
 Mchekeshaji huyo ambaye alikuwa akishiriki katika filamu mbali mbali za ucheshi alianza kuonekana kupitia kituo cha televisheni cha Chanel TEN katika kipindi cha vituko show.
Image result for kinyambe
Kinyambe enzi za uhai wake akiwa katika harakati za kuigiza pamoja na mkongwe Mzee Jangala
Image result for kinyambe
Kinyambe enzi za uhai wake akiwa katika harakati za kuigiza pamoja na msanii Matumaini
Kinyambe atakumbukwa zaidi kwa aina pekee ya uigizaji aliokuwa akiufanya kiasi cha kuweza kujikusanyia mashabiki lukuki nchini.
 Tutazidi kuwajuza zaidi kuhusu hili.    R.I.P KINYAMBE


Hapa chini ni moja kati ya kazi za sanaa alizofanya Kinyambe

  1 comment:

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA