Saturday 10 May 2014

NI ZAIDI YA LAANA, MFANYA BIASHARA MAARUFU AFUMANIWA AKIMRA URODA (KUMLAWITI) SHOGA


OFM walivyomnasa mfanyabiashara wa magari (kushoto) chumbani akitaka kumlawiti modo maarufu.
EEH Mungu! Unaweza kukataa lakini ni ukweli kwamba dunia imekwisha! Mambo yanayotendeka kila kukicha juu ya ardhi yanathibitisha hilo.
Mfanyabiashara maarufu wa magari jijini Dar es Salaam aliyefahamika kwa jina la Juvenali amekumbwa na aibu ya mwaka baada ya kunaswa mtupu chumbani na mmoja wa wabunifu wa mavazi ‘modo’ maarufu Bongo (jina tunalihifadhi kwa sasa kwa sababu za kimaadili).
...amefungwa pingu.
Tukio hilo la aibu lilimkuta mfanyabiashara huyo nyumbani kwake, Mbezi ya Tangi-Bovu jijini Dar es Salaam hivi karibuni ambapo wawili hao walinaswa chumbani wakiwa watupu katika mtego maalum.

KISA KILIPOANZIA
Chanzo cha kufichuka kwa taarifa hizo ni modo huyo kumwonesha kaka yake (naye jina tunalo) meseji ‘tamutamu’ kutoka kwa mfanyabiashara huyo kwenda kwake akimshawishi kumlawiti.

KAKA MTU ACHARUKA
Ilidaiwa kuwa kaka mtu alikasirika, aliamini kitendo cha mfanyabiashara huyo kutaka kumlawiti mdogo wake ni kuidhalilisha familia.
“Kaka akamwambia mdogo wake kwamba ni lazima wamtege jamaa huyo ili kumshikisha adabu na ache tabia hiyo,” kilisema chanzo.
                               ...Akitatiwa na Polisi.
KAKA ACHUKUA GAZETI, APIGA SIMU OFM
Baada ya kukubaliana na mdogo wake, kaka huyo alitafuta Gazeti la Amani na kukutana na namba za Kamanda wa Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ na kuzipiga.
Kaka: Jamani poleni na kazi, hapo ni OFM?
OFM: Tumepoa ndugu, ndiyo sisi, tena unaongea na mimi kamanda mwenyewe. Niambie ndugu yangu, bila shaka unataka kutupatia kazi, tupo tayari.
Kaka: Ni kweli, kuna jamaa mmoja ni mfanyabiashara wa magari, anamtumia meseji mdogo wangu akimshawishi amlawiti. Tukio hili limenikera sana. Naomba tukutane ili tupange jinsi ya kumnasa ili kukomesha tabia hii.
Nimeshazungumza na mdogo wangu na yupo tayari kwa jambo hilo ili tumtege, tukamilishe hiyo kazi kukomesha huu upuuzi.
OFM: Sawa kabisa, inawezekana.
Kilichoendelea hapo ilikuwa ni OFM kumpa baadhi ya maelekezo kaka mtu, wakakubaliana kila kitu namna mchezo ambavyo ungekamilika kwa mbinu za kitaalam za makachero wa OFM.
        ...Mfanyabiashara  huyo akichukuliwa na polisi.
OFM YAPOKEA KAZI, YARIPOTI POLISI
Baada ya kukutana na kaka wa modo huyo na kupanga kila kitu, OFM iliwasiliana na Jeshi la Polisi Kituo cha Mbezi - Makonde, Dar ambapo taarifa za uovu huo zilikuwa na dalili ya kufanyika karibu na maeneo hayo.
Mkuu wa kituo hicho alitoa ‘vijana’ wake wawili, shupavu waliojitambulisha kwa majina ya Afande Nassoro na Afande Sele. Wakakamavu kabisa.
    
    ...Safari ya kuelekea kituo cha polisi cha Kawe.
KATIKA ENEO LA TUKIO
Fasta, OFM na askari hao walielekea Mbezi Tangi - Bovu, kituo cha daladala eneo la mtego ambapo mfanyabiashara huyo alimuahidi kijana huyo akamchukulie hapo kwenda naye kwenye nyumba ya kumfanyia usodoma.

MFANYABIASHARA AFIKA NA GARI
Wakiwa mita kadhaa, OFM na polisi, walimuona mfanyabiashara huyo akiwasili na gari aina ya GX 100 (namba za usajili tunazo). Alifunga breki miguuni kwa kijana huyo, akamfungulia mlango, naye akazama ndani.
Safari ilianza kuelekea upande wa Bagamoyo lakini mita chache gari hilo lilikata kulia. OFM na maafande walikuwa wakifuatilia kwa nyuma bila kujulikana.
                        ...Akiwa kituo cha polisi.
GARI LAFIKA NYUMBA YA TUKIO
Baada ya mwendo wa kama kilometa mbili, gari hilo lilifika kwenye nyumba  moja na kupiga honi kisha geti  likafunguliwa, gari likaingia na geti likafungwa.

MODO NDANI YA CHUMBA CHA TUKIO
OFM, maafande wakiwa nje, wawili hao tayari walikuwa chumbani ambapo dogo huyo aliwasiliana na ‘makachero’ wa nje na kuwaambia kwamba mfanyabiashara huyo alishasaula nguo na yupo kama alivyozaliwa, alikuwa katika hatua za awali za kutaka kukamilisha ufirauni wake. Hapo sasa OFM na polisi wakajipanga kuchoma ndani kuzuia unyambisi huo.

KIZINGITI
Hata hivyo, OFM na askari hao walishindwa kuingia baada ya geti kufungwa kwa ndani na aliyefunga kutoka nje kwa kutumia mlango mwingine.
Hata hivyo, askari walitumika ukomandoo, ‘timu’ ikafanikiwa kuzama ndani moja kwa moja na kwenda kugonga katika chumba husika (wale askari hatari sana aiseee!).

AFUNGUA MLANGO BILA WASIWASI
Bila kujua kuwa OFM na polisi ndiyo waliogonga mlango,  jamaa huyo alifungua mlango na kukutwa akiwa mtupu sanjari na modo huyo.

SHETANI ATUPIWA ZIGO
Maafande walimuuliza ‘biznesmani’ huyo ni kwa nini wamekutwa uchi tena wanaume watupu chumbani, alijibu kuwa walikuwa wanahisi joto ndiyo maana waliamua kuvua nguo zote.

Lakini akaongeza: “Jamani niacheni. Hii ni aibu, nitawapeni chochote kile mnachotaka, shetani ndiye alinipitia jamani.”

SAFARI KUELEKEA LUPANGO
Mfanyabiashara huyo alichukuliwa na askari hao hadi polisi lakini baadaye akahamishiwa Kituo cha Kawe ambako shauri hilo liliandikishwa na kupewa jalada la kesi namba KW/RB/1747/2014.
Baada ya kuchukuliwa maelezo, mfanyabiashara huyo aliswekwa lupango akisubiri sheria kuchukua mkondo wake.

OFM
OFM kama ilivyotambulishwa awali, ipo kwa ajili yako wewe Mtanzania unayeona uovu katika jamii na vyombo husika vikashindwa kuchukua hatua, kwa OFM kila kitu kinawezekana! Wanaweza kuingia popote na kuchunguza uovu wowote kwa mafanikio makubwa – tuletee kazi tutaifanya.
na GPL

  3 comments:

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA