Tuesday, 14 June 2016

CUF WASHITUKIA KIGEU GEU CHA PROF. LIPUMBA


Na Julius Mathias-Mwananchi 


Dar es Salaam. Kama ulidhani ‘mtiti’ wa watu aliotinga nao aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba makao makuu ya chama hicho, Buguruni jijini Dar es Salaam ungemsaidia kurejesha nafasi yake hiyo, basi umekosea.

Profesa Lipumba aliyetengua uamuzi wake wa kung’atuka kwenye wadhifa huo na kuomba kurejea madarakani, amekumbana na kizuizi cha viongozi wa juu wa chama hicho ambao wamepinga hatua hiyo wakisema katiba haimruhusu na nakwenda kukiua chama.

Awali, msomi huyo alitangaza nia ya kurejea uongozini jana kwenye ofisi za makao makuu ya chama hicho, huku akibainisha kuwa amefanya hivyo baada ya kuombwa.


Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA