Saturday 11 June 2016

UFARANSA YAANZA KWA USHINDI EURO 2016


Olivier Giroud wheels away in celebration after scoring the opening goal of this year's European Championship in France
WENYEJI wa michuano ya UEFA EURO 2016, timu ya Taifa ya Ufaransa wameianza vema michuano hiyo baada ya kuitandika Romania mabao 2-1 kwenye dimba la Stade de France.

Ufaransa walianza kupata bao katika dakika ya 56 lililowekwa nyavuni na straika wa Arsenal, Olivier Giroud akimalizia kwa kichwa krosi ya Dimitri Payet.
Payet's strike heads towards the back of the net to win the game for the Euro 2016 hosts at the Stade de France
Katika dakika ya 64 beki wa Ufaransa, Patrice Evra alimfanyia madhambi mshambuliaji wa Romania, Stanciu katika eneo la 18 hivyo mwamuzi akaamuru ipigwe penati iliyowekwa nyavuni na Stancu.

Payet ndiye aliyeihakikishia Ufaransa pointi tatu muhimu baada ya kufumua shuti kali la mguu wa kushoto lililojaa moja kwa moja nyavuni.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA