UZALISHAJI WA KUTUMIA PUMBA ZA MPUNGA WAIWEZESHA TBL MWANZA KUJINYAKULIA TUZO YA MACKAY
Mkurugenzi wa ufundi wa TBL Group, Gavin Van Wijk akiongea na waandishi wa habari na wafanyakazi wa TBL Mwanza wakati wa hafla a kukabidhi tuzo |
Kiwanda cha TBL Mwanza
kilichopo chini ya TBL Group na kikiwa moja ya kiwanda kinachoshikilia rekodi
ya ubora katika viwanda vya SABMiller duniani kimeshinda tuzo kubwa
ya Mackay kutokana na kufanya uzalishaji kwa kutumia pumba za mpunga.
Meneja Msaidizi wa TBL Mwanza,Gabriel Pitso,akipokea tuzo kutoka kwa Mkurugenzi wa ufundi Gavin Van Wijk |
Malengo ya SABMiller ambayo
baadhi yake yanashahabiana na malengo ya Umoja wa Mataifa yamelenga katika
kufanya uzalishaji usio na athari kwa mazingira na unaoleta mabadiliko kwa
jamii kwa kuziwezesha kujikwamua kimapato.
Akiongea
baada ya kukabidhi tuzo hiyo kwa uongozi na wafanyakazi wa TBL
Mwanza,Mkurugenzi wa Ufundi wa TBL Group, Gavin Van Wijk,amekipongeza kiwanda
kwa kuendelea kungaa na kujinyakulia tuzo mbalimbali kama hii ya
Mackay.“Ushindani ulikuwa mkubwa na ulihusisha viwanda
mbalimbali lakini hatimaye mmefanikiwa kunyakua tuzo hii na kuweka
rekodi ya kuwa kiwanda cha kwanza kuipata barani Afrika”.Alisema
Alitoa shukrani kwa wateja
wote wanaoendelea kuiunga mkono kampuni kwa kununua bidhaa zake na kuongeza
kuwa siku zote kampuni itahakikisha inaongeza uzalishaji na kuingiza
bidhaa bora sokoni ikiwemo kusaidia huduma mbalimbali zinazoleta mabadiliko
kwenye jamii.
Akiongea juu ya tuzo hii
katika hafla ya kuipokea iliyofanyika kiwandani Mwanza ,Meneja wa kiwanda hicho
Gabriel Pitso, alisema kuwa kiwanda hicho ndicho cha kwanza kupata tuzo hii
nchini na ushindi huu umetokana na kufanya uzalishaji unaozingatia utunzaji wa
mazingira kwa kutumia mashine zinazotumia pumba za mpunga na mashudu ambao
kitaalamu hujulikana kama Dry –De- Husking (DDH) .
Alisema kampuni mama ya
SABMiller ilifanya utafiti na baada ya utafiti huo iliamua kabla ya kuanzisha
teknolojia ya uzalishaji usiotumia mafuta ya dizeli
kwenye viwanda vyake vyote ianzie katika kiwanda cha Mwanza ambapo katika miaka
ya kwanza ya majaribio mafanikio makubwa yamepatikana kutokana na kutumia
teknolojia hii ikiwemo kupunguza gharama za uendeshaji na kupunguza uharibifu
wa mazingira.
Mbali na kupunguza athari
za uharibifu wa mazingira na gharama za uendeshaji teknolojia hii kwa kiasi
kikubwa inasaidia kuongeza vipato kwa wakulima wa pamba na mchele na
wafanyabiashara wanaokusanya pumba kwa ajili ya kukiuzia kiwanda “Zamani pumba
za mchele zilikuwa takataka lakini hivi sasa zimegeuka lulu kwa kuwa zina soko
tunazitumia katika uzalishaji hivyo kuna wafanyabiashara wanapita maeneo
mbalimbali wakizikusanya kwa ajili ya kutuuzia na huu ndio uwekezaji mzuri
unaonufaisha jamii inayoishi jirani na maeneo ya kiwanda na ni moja
ya malengo yetu”.Alisema.
0 comments:
Post a Comment