Sunday 17 July 2016

WAFANYAKAZI WA TBL MWANZA WASHEREKEA TUZO YA UZALISHAJI WA KUTUMIA PUMBA ZA MPUNGA

 Mwakilishi wa Wafanyakazi Tuico katika Kiwanda cha Bia TBL mkoani Mwanza, Vedasia Mafuru akizungumza wakati wa hafla hiyo
 Baadhi ya wafanyakazi wakiwa kwenye picha ya pamoja katika sherehe ya wafanyakazi kusherekea tuzo kubwa ya Mackay waliyoipata kutokana na kiwanda kufanya uzalishaji wa kutumia pumba za mpunga
 Meneja wa Kiwanda cha Bia(TBL) mkoani Mwanza, Gabriel Pitso akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati waherehe hiyo
 Aliyekuwa Meneja wa kiwanda cha Bia TBL mkoani Mwanza, Richmond Raymond akimkabidhi tuzo Meneja wa Kiwanda hicho, Gabriel Pitso katika sherehe ya wafanyakazi kusherekea tuzo kubwa ya Mackay waliyoipata kutokana na kufanya uzalishaji wa kutumia pumba za mpunga
 Aliyekuwa Meneja wa kiwanda cha Bia TBL mkoani Mwanza, Richmond Raymond akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa sherehe
Baadhi ya wafanyakazi wakifuatilia matukio wakati huo wakiburudika

Wafanyakazi wa kiwanda cha TBL Mwanza kilichopo chini ya TBL Group jana walisheherekea mafanikio waliyoyapata mwaka huu ikiwemo  kushinda tuzo kubwa ya Mackay kutokana na kufanya uzalishaji wa kutumia teknolojia ya pumba za mpunga .
 
Mackay ni tuzo kubwa ya SABMiller ya kumuenzi mmoja wa Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo Graham Mackay ambaye katika kipindi chake cha kuitumikia kampuni hiyo aliendeleza kwa kiasi kikubwa na alifariki miaka mitatu iliyopita ambapo kampuni imeanzisha tuzo yake kwa viwanda vyake ambavyo vinafanya uzalishaji unaoendana sambamba na malengo ya kampuni .
 
Moja ya malengo ya SABMiller ambayo baadhi yake yanashahabiana na malengo ya Umoja wa Mataifa yamelenga katika kufanya uzalishaji usio na athari kwa mazingira na unaoleta mabadiliko kwa jamii kwa kuziwezesha kujikwamua kiuchumi.
 
Akiongea katika hafla hiyo,aliyekuwa Meneja wa kiwanda hicho ambaye amehamishiwa kikazi nchini Afrika ya Kusini,Richmond Raymond amewapongeza wafanyakazi wote kwa mafanikio haya kwa kukiwezesha kiwanda  kuendelea kungaa na kujinyakulia tuzo  mbalimbali kama hii ya Mackay.“Ushindani ulikuwa mkubwa na ulihusisha viwanda mbalimbali lakini hatimaye tumefanikiwa kunyakua tuzo hii na kuweka rekodi ya kuwa kiwanda cha kwanza kuipata barani Afrika”.Alisema
 
Pia alitoa shukrani kwa wateja wote wanaoendelea kuiunga mkono kampuni kwa kununua bidhaa zake na kuongeza kuwa siku zote kampuni itahakikisha inaongeza  uzalishaji na kuendelea kuingiza bidhaa bora sokoni ikiwemo kusaidia huduma mbalimbali zinazoleta mabadiliko kwenye jamii.
 
Kwa upande wake Meneja wa TBL Mwanza Gabriel Pitso, alisema kuwa kiwanda hicho ndicho cha kwanza kupata tuzo hii nchini na ushindi huu umetokana na kufanya uzalishaji unaozingatia utunzaji wa mazingira kwa kutumia mashine zinazotumia pumba za mpunga na mashudu ambao kitaalamu hujulikana kama Dry –De- Husking (DDH)  .
 
Alisema kampuni mama ya SABMiller ilifanya utafiti na baada ya utafiti huo iliamua kabla ya kuanzisha teknolojia  ya uzalishaji usiotumia mafuta  ya dizeli kwenye viwanda vyake vyote ianzie katika kiwanda cha Mwanza ambapo katika miaka ya kwanza ya majaribio mafanikio makubwa yamepatikana kutokana na kutumia teknolojia hii ikiwemo kupunguza gharama za uendeshaji na kupunguza uharibifu wa mazingira.
 
Mbali na kupunguza athari za uharibifu wa mazingira na gharama za uendeshaji teknolojia hii kwa kiasi kikubwa inasaidia kuongeza vipato kwa wakulima wa pamba na mchele  na wafanyabiashara wanaokusanya pumba kwa ajili ya kukiuzia kiwanda “Zamani pumba za mchele zilikuwa takataka lakini hivi sasa zimegeuka lulu kwa kuwa zina soko tunazitumia katika uzalishaji hivyo kuna wafanyabiashara wanapita maeneo mbalimbali wakizikusanya kwa ajili ya kutuuzia na huu ndio uwekezaji mzuri unaonufaisha jamii inayoishi jirani na maeneo ya kiwanda na  ni moja ya malengo yetu”.Alisema.

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA