Monday 1 August 2016

PICHA:JOSEPH SENGA AZIKWA NYUMBANI KWAO KWIMBA MKOANI MWANZA

Waombolezaji wakilishusha jeneza lenye mwili wa marehemu Joseph Senga, aliyekuwa mpiga picha mkuu wa gazeti la Tanzania Daima, wakati wa mazishi yake yaliyofanyika Mchana wa leo kwenye Makaburi ya Kijijini kwao, Shushu wilayani Kwimba mkoani Mwanza. Marehemu Senga alifariki wiki iliyopita nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu ya moyo. Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi AMIN.
Mjane wa Marehemu Joseph Senga, Bi. Winfrida Senga akiweka shada la maua kwenye Kaburi la Mumewe, wakati wa mazishi yaliyofanyika Mchana wa leo kwenye Makaburi ya Kijijini kwao, Shushu Kwimba, Jijini Mwanza.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Mpigapicha Mkuu wa gazeti hili, marehemu Joseph Senga wakati wa mazishi yake yaliyofanyika katika Kijiji cha Shushi Wilaya ya Kwimba, Mwanza. 
Mbunge wa Jimbo la Sumve, Richard Ndassa akiweka shada la Maua.
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe, ambaye pia ni Mmiliki wa Kampuni ya FreeMedia wachapishaji wa Gazeti la Tanzania Daima alikokuwa akifanya Kazi Marehemu Joseph Senga, akitoa salamu za Rambirambi, wakati wa Mazishi yaliyofanyika Mchana wa leo kwenye Makaburi ya Kijijini kwao, Shushu Kwimba, Jijini Mwanza.
Ibada ya Mazishi ikiendelea.
Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima, Neville Meena akiweka shada la maua kaburini.
Credit Michuzi jr

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA