SHAMRASHAMRA KIBAO ZAPAMBA UFUNGUZI WA MICHUANO YA OLIMPIKI 2016
Michuano ya Michezo ya Olimpiki mwaka 2016 imefunguliwa rasmi kwa shamrashamra za aina yake Jijini Rio katika dimba la Maracana nchini Brazil.
Tukio hilo lililorushwa mubashara kupitia runinga kwa watu bilioni 3 duniani, liliambatana na kuonyesha historia, utamaduni na uzuri wa Brazil.
Katika ufunguzi huo mwanariadha wa zamani wa Vanderlei de Lima aliwasha Mwenge wa Olimpiki, na mwanariadha wa zamani Kenya Kipchoge Keino alinyanyua juu kombe la Olimpiki mwishoni wa sherehe hizo za ufunguzi.
Dimba la Maracana lilivyokuwa linaonekana wakati wa shamrashamra za ufunguzi wa michuano ya olimpiki
Kikundi cha dansi cha Samba kikitoa burudani wakati wa ufunguzi
Burudani ya samba ikiendelea kutolewa wakati wa ufunguzi wa michuano ya Olimpiki
Rais wa mpito wa Brazil Michel Temer akihutubia wakati wa ufunguzi wa michuano hiyo
Mwanariadha wa zamani wa Brazil Vanderlei de Lima akiwasha Mwenge wa Olimpiki
0 comments:
Post a Comment