Monday 6 July 2015

TANZANIA BREWERIES LIMITED YAHAMASISHA WASOMI KUJIPANGA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA SOKO LA AJIRA


Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Roberto Jarrin akielezea namna TBL inavyopiga hatua katika uendeshaji na utoaji wa huduma zake nchini Tanzania 
Mkurugenzi  mtendaji wa kampuni  ya TBL Ndugu Roberto Jarrin ameendesha warsha wa kibiashara katika chuo kikuu cha kumbukumbu ya Stefano Moshi kampasi ya mjini mwanzoni mwa mwezi huu.

Akiwa mzungumzaji mkuu katika warsha hiyo iliyohudhuriwa na waadhiri,wafanya kazi pamoja na wanafunzi wa chuo hicho,mkurugenzi mtendaji huyo aliye ambatana na meneja wa mambo ya nje na mawasiliano TBL Bi Emma Oriyo na afisa masoko TBL kanda ya kaskazini mashariki Ndugu Devis Deogratius, alianza kwa kutambulisha bidhaa mbalimbali  ambazo zinatengenezwa na kampuni hiyo na kuonesha namna TBL inavyopiga hatua katika kujikuza kama kampuni.

Baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha kumbu kumbu ya Stefano Moshi wakisikiliza kwa makini Mkurugenzi wa TBL Roberto Jarrin
Akielezea kuhusu masoko Ndugu Jarrin alielezea namna kampuni hiyo inavyojiendesha katika nchi za Afrika pamoja na aina za bidhaa kulingana na maeneo husika ikiwa ni pamoja na changamoto wanazokutana nazo na namna kampuni inavyokabiliana nazo na hasa ikiwa ni upatikanaji wa malighafi kutoka kwa wakulima akitoa mfano kuwa Uganda ndiyo nchi inayoongoza kwa uzalishaji wa malighafi katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Taswira ya ukumbi  na wahudhuriaji ilivyokuwa wakati wa warsha hiyo 

Akijibu maswali ya wanafunzi waliotaka kujua namna TBL inavyotoa nafasi za ajira kwa wasomi na jinsi kampuni inavyolichukulia suala la rushwa katika utoaji wa ajira Ndugu Jarrin alisema “TBL inathamini wasomi wa nchi hii na inawapa nafasi ya kuonesha uwezo wao wa kazi katika kwa njia za tarajali lakini pia mpaka sasa imeweza kutoa ajira kwa  zaidi ya watanzania 100,000, Vile vile kuhusu rushwa hili ni tatizo lenye sura ya kipekee tunajitahidi kama kampuni kuajiri mtu kwa kuwa anambinu za kazi na sii vinginevyo”.

Afisa masoko TBL kanda ya kaskazini mashariki  Devis Deogratius akizungumzia mchakato wa ajira kwa wasomi nchini Tanzania
Akikazia kuhusu maelezo hayo afisa masoko TBL kanda ya kaskazini mashariki Ndugu Devis Deogratius alisema kuwa wasomi wengi wanajisahau kuwa elimu wanazopata hazitoshi wao kuonekana bora katika ushindani wa soko la ajira hivyo wanahitaji kuweka jitihada zaidi  katika kujishighulisha na kudhihirisha ubora wao katika utendaji huku akitoa mfano wake kwa namna alivyoajiriwa na TBL mwaka 2007 na kwa jitihada na nidhamu ya kazi aliyoonesha aliweza kuendelezwa kielimu nchini Afrika ya kusini na sasa kuwa  afisa masoko TBL kanda ya kaskazini mashariki.

Mhadhiri wa chuo kikuu cha kumbu kumbu ya Stefano Moshi Dr.Gasper mpehongwa akitoa neno la shukrani wakati wa warsha hiyo


Akizungumzia warsha hiyo mhadhiri wa chuo kikuu cha kumbukumbu ya Stefano Moshi Dr.Gasper Mpehongwa alishukuru na kusifu ushirikiano uliopo kati ya TBL na chuo hicho  kwa kuleta elimu hii chuoni hapa “Elimu iliyotolewa kupitia warsha hii imekuja katika kipindi kizuri hasa ambapo wanafunzi walikuwa wakijiuliza namna ya kupambana na soko la ajira ,ni matumaini yangu mbegu hii iliyopandwa katika fikra za wanafunzi hawa itazaa matunda mema”.

Victor Kajuna mwanafunzi mwaka wa tatu akimuuliza swali  Mkurugenzi mtendaji wa TBL Roberto Jarrin katika warsha hiyo


Victor Kajuna mwanafunzi mwaka wa tatu alipongeza kampuni ya TBL kwa hatua iliyopiga na kufanikiwa kugusa maisha ya watanzania wengi kupitia huduma zake na kwa kuwa na mchango mkubwa kwa pato lataifa kupitia kodi huku.Sambaba na hilo Sebastian Femba mwanafunzi mwaka wa aliesema kuwa warsha hii licha ya kumpa nafasi ya kuifahamu TBL kwa upana imempa changamoto ya kujituma hususani akijipanga kukabiliana na ajira pindi atakapohitimu masomo yake.

Meneja wa mambo ya nje na mawasiliano TBL Bi Emma Oriyo akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kwa warsha hiyo
Alipokuwa akizungumzia suala la kujipanga na changamoto za ajira kwa wasomi meneja wa mambo ya nje na mawasiliano TBL Bi Emma Oriyo alisema “ili kuwa na mafanikio katika soko la ajira ni kujijiengea uwezo wa haraka kumudu mabadiliko ya fikra kwani hilo litakutofautisha wewe na wengine”.
Mkurugenzi mtendaji wa TBL Roberto  Jarrin akizungumza na mmoja wa wahudhuriaji wa warsha hiyo mara baada ya kumalizika 

Meneja wa mambo ya nje na mawasiliano TBL Bi Emma Oriyo akiwa na Mhadhiri wa chuo kikuu cha kumbu kumbu ya Stefano Moshi Dr.Gasper mpehongwa wakielezea uhusiano uliopo baina ya TBL na chuo hicho

Mwanafunzi wa mwaka wa pili chuo kikuu cha kumbu kumbu ya Stefano Moshi Frank Chang'a akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi 
Warsha hiyo ni ya kwanza kufanyika chuoni  hapo kwa kushirikisha waadhiri,wafanya kazi pamoja na wanafunzi wa chuo hicho na imekuja kufuatia ushirikiano uliopo kati ya TBL na chuo cha Stefano Moshi uliodumu kwa takribani miaka nane sasa.

Na Dickson Mulashani wa FUNGUKA LIVE BLOG

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA