Friday 21 April 2017

EUROPA:: CELTA VIGO YAFUZU HATUA YA NUSU FAINALI ,GENK YA SAMATTA YAKWAMA


Celta Vigo imetinga nusu fainali ya Ligi ya Uropa na kuitoa timu ya Mbwana Samatta ya Genk kwa ushindi wa magoli ya jumla 4-1, baada ya jana kutoka sare ya 1-1.

Celta Vigo ilikuwa ishapata ushindi wa magoli 3-2 katika mchezo wa awali dhidi ya Genk na kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.

Katika mchezo wa jana Pione Sisto alikuwa wa kwanza kuifungia goli Celta Vigo katika dakika ya 63 lakini Leandro Trossard alisawazisha dakika nne baadaye.
                     Pione Sisto akiachia shuti na kuifungia Celta Vigo goli katika mchezo huo
Leandro Trossard akishangilia baada ya kuifungia Genk goli la kusawazisha huku Mbwana Samatta akiangalia

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA