18:50 |
|
Marekani inapeleka wanajeshi zaidi ya mara mbili ya kikosi cha operesheni maalum kusaidia kumtafuta mbabe wa vita Joseph Kony. Rais Barack Obama aliamuru kiasi cha wanajeshi 150 na angalau ndege nne za CV-22 kuelekea Uganda siku ya Jumapili ambapo ni mara ya kwanza kwa Marekani kupeleka ndege za kijeshi kumtafuta Kony na wapiganaji wake. Msako unalenga kwenye misitu inayopakana na Jamhuri ya Afrika ya kati, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC. Bwana Obama awali alipeleka kiasi cha wanajeshi 100 wa kikosi maalumu cha Marekani kuelekea kwenye eneo hilo mwaka 2011 ambako wamekuwa wakiwasaidia wanajeshi 5,000 wa kikosi cha operesheni za kieneo wa Umoja wa Afrika.
Pentagon inasema wanajeshi wa Marekani wana jukumu la kutoa taarifa na msaada na wanatumia silaha kwa kujilinda. Kony anatafutwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu-ICC kwa makosa 33 ya uhalifu wa vita na uhalifu dhidi ya binadamu. Aliendesha vita vikali vya msituni dhidi ya serikali la Uganda kwa takribani miongo miwili kabla ya kukimbia na wapiganaji wake kuelekea kwenye misitu ya Afrika ya kati katika mwaka 2005. Kony anaaminika kuwa na wapiganaji wachache waliobaki nae.
Related Posts:
USIFAKAMIE MAPENZI ETI UNAONDOA ‘STRESS’
KARIBU mpenzi msomaji tupeane elimu ya mapenzi ambayo tunaamini ‘yana-rani’ dunia. Wiki iliyopita tulizungumzia mpenzi ambaye akipendwa ina… Read More
VIDEO: MAHOJIANO YA BBC NA MGOMBEA URAIS WA UKAWA, MH. EDWARD NGOYAI LOWASSA - OKTOBA 21, 2015
Zuhura Yunus alimhoji Lowassa akiwa nyumbani kwake Monduli, Arusha na kwanza akataka maelezo zaidi kuhusu kipaumbele chake cha elimu.
Mahoji… Read More
WATOTO WA PELE WOTE WACHEKA NA NYAVU, ANDRE AIPA USHINDI SWANSEA IKIIMALIZA ASTON VILLA 2-1
Jordan Ayew akishangilia baada ya kuipa Aston Villa bao
Andre Ayew akishangilia mara baada ya kufunga bao la ushindi
Andre Ayew amefunga ba… Read More
TUPIGE KURA, TUPOKEE MATOKEO KWA AMANI NA UTULIVU, KUNA MAISHA BAADA YA UCHAGUZI
JUMAPILI ya Oktoba 25, 2015, Tanzania inafanya Uchaguzi Mkuu wa madiwani, wabunge pamoja na kumpata Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano … Read More
MAKAMU WA RAIS WA MALDIVES AKAMATWA
Makamu wa Rais wa Maldives, Ahmed Adeeb leo amekamatwa akituhumiwa kutaka kumuua rais wake, Abdulla Yameen.
MAKAMU wa Rais wa Maldives, Ahmed… Read More
0 comments:
Post a Comment