Monday 24 March 2014

Refa ajutia kadi nyekundu kwa Arsenal




Refa wa mchezo kati ya Chelsea na Arsenal akitoa kadi kimakosa
Refa Andre Marriner huenda akawekwa kando kwenye michezo ya mwishoni mwa juma baada ya kufanya makosa kwenye michuano ya ligi kuu kumwondoa kimakosa mchezaji wa Arsenal wakati timu hiyo ilipopoteza mchezo kwa kuchapwa magoli 6-0 na Chelsea.
Marriner alitoa Penalti wakati wa mchezo wa siku ya Jumamosi baada ya Alex Oxlade-Chamberlain kushika mpira, lakini Kieran Gibbs aliondolewa kimakosa
Oxlade-Chamberlain alionekana akimwambia Refa kuwa yeye ndiye aliyeshika mpira, hata hivyo uamuzi wa awali ndio ulikua wa mwisho.
Hata hivyo baadae Mariner alikiri na kuomba radhi kwa makosa yaliyojitokeza, akikiri kufanya makosa kutomtambua aliyepaswa kuadhibiwa katika mchezo huo.
Chama cha waamuzi wa mchezo wa kulipwa kimesema kuwa matukio ya kumwadhibu mchezaji kimamkosa ni nadra kutokea na mara nyingi husababishwa na sababu mbalimbali za kiufundi
na BBC

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA