Saturday 29 March 2014

Robert Mugabe kuususia mkutano kati ya Umoja wa Afrika na Umoja wa Ulaya endapo mkewe hataalikwa

Serikali ya Zimbabwe imeeleza kuwa rais Robert Mugabe ataususia mkutano uliopangwa kufanyika mwanzoni mwa April kati ya Umoja wa Afrika (AU) na Umoja wa Ulaya (EU) endapo mkewe Grace hataalikwa.
Mkutano huo utafanyika Brussels, Ubeligiji (katika bara la Ulaya) ikizingatiwa kuwa mwaka 2002 Umoja wa Ulaya uliwawekea vizuizi Robert Mugabe na mkewe Grace kutozitembelea nchi za bara la Ulaya.
Mugabe ambaye ni makamo mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) amepewa mualiko wa kuhudhuria mkutano huo lakini mkewe hakupewa mualiko huo.

“Ni kitu cha kushangaza kwamba EU haikutoa mualiko kwa First Lady. Kitu ambacho Mungu amekiweka pamoja EU inataka kukitenga. Hivi wanatarajia rais aiheshimu EU na kuikosea heshima ndoa yake mwenyewe?” alikaririwa msemaji wa Mugabe, George Charamba.
Mke wa Mugabe alikuwa akikosolewa kuwa hutumia pesa nyingi kufanya manunuzi ya anasa kila anapolitembelea bara la Ulaya.
NA wananchi blg

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA