Sunday, 18 May 2014

DEREVA AKIMBIA GARI LAKE MCHANA KWEUPE

Na KD MULA
Moshi.
Dereva  ambaye jina lake halikufahamika kwa haraka ametelekeza gari lake baada ya kukimbizwa na askari polisi jana  majira ya saa tano.
Chanzo cha habari kimeeleza kuwa dereva huyo alisimamishwa na askari wa usalama barabarani ili waweze  kulikaguwa gari hilo lakini alikiuka agizo hilo na kukimbia lakini polisi huyo aliweza kutoa taarifa haraka kwa askari wenzake na kuanza kumfuata dereve huyo kwa kutumia usafiri wa pikipiki
Walipofika maeneo ya Mbuyuni dereva huyo alishindwa mchaka mchaka huo na kushuka ndani ya gari akikimbilia pasipojulikana.
Askari polisi hao walisema kuwa gari  ya dereva huyo ilikuwa na makosa mengi sababu iliyomfanya  kugoma kusimama pale aliposimamishwa na askari wa usalama barabarani maarufu kama traffic moja ya kosa alikuwa nalo ni kutolipa mapato ya TRA
“Baada ya kupata taarifa kutoka kwa askari wa barabani na kututajia namba ya gari hilo sisi tulianza kulitafuta na kuanza kulifukuzia kwa nyuma lakini ilipofika maeneo ya mbuyuni dereve huyo aliweza kushuka ndani ya gari na kulikimbia gari lake” alisema mmoja wa askari waliohusika na operesheni hIyo (jina kapuni). 
CREDIT(PICHA) MOHAMED MGANGA

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA