Thursday 8 May 2014

MFAHAMU HELEN COSTA: KOCHA WA KWANZA MWANAMKE KUFUNDISHA KLABU YA WANAUME ULAYA


http://www.dohastadiumplusqatar.com/wp-content/uploads/2011/08/woman-football-coach.jpg

Aliyekuwa kocha wa timu ya taifa ya wanawake ya Irani na Qatar, Helena Costa ametengeneza historia mpya kwenye soka nchini barani ulaya.
Klabu ya ligi daraja la kwanza ya Ufaransa Clermont imeweka historia mpya kwenye soka la nchi hiyo kwa kumtangaza mwanamama Helena Costa kuwa kocha wao mpya kuanzia msimu ujao, na kumfanya kuwa mwanamke wa kwanza kufundisha soka la hadhi ya juu nchini Ufaransa.
Costa, 36, alikuwa kocha wa timu ya taifa ya wanawake ya Irani tangu mwaka 2012 lakini sasa amekubali kumrithi Regis Brouard kwenye klabu ya Clermont.
Helena ambaye ni raia wa Ureno, aliwahi kufanya kazi kama kocha mkuu wa kituo cha soka cha klabu ya Benfica na timu kadhaa nyingine nchini Ureno, ambapo aliweza kushinda makombe kadhaa. Pia aliwahi kuifundisha timu ya wanawake  ya taifa ya Qatar.
NA MATUKIO BLG

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA