Waziri wa Usalama wa taifa wa Somalia ajiuzulu
Waziri wa
Usalama wa Taifa wa Somalia amejiuzulu. Abdikarim Hussein Guled
amejiuzulu baada ya kujiri shambulio la kigaidi karibu na bunge la
Somalia mjini Mogadishu hapo jana.
Taarifa
zinasema kuwa, baada ya shambulio hilo lililopelekea watu 10 kuuawa,
waziri huyo wa usalama wa Somalia alishinikizwa na wabungen ajiuzulu.
Wakati
huo huo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelaani shambulio hilo
lililofanywa na wanamgambo wa al Shabab kwenye jengo la bunge la
Somalia.
Wajumbe
wa Baraza la Usalama wamesema kuwa wanasikitishwa na shambulio hilo
dhidi ya bunge taasisi ambayo inawakilisha wananchi wa Somalia, na
ambako ni mahala wanapotumaini kupata usalama, amani na maendeleo kwa
njia halali.

0 comments:
Post a Comment