Sunday 15 June 2014

England yaanza vibaya kombe la dunia.....Yachapwa 2-1 na Italia,, Uruguay yakalia kuti la Moto....Yachapwa 3-1 na Costa Rica, Suarez akalia benchi mwanzo mwisho





Straika wa Italia, Mario Balotelli (kushoto) akiifungia timu yake bao la ushindi dhidi ya England usiku huu.


Timu  ya Taifa ya England  imeanza vibaya kombe la dunia baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya timu ya Taifa ya Italia maarufu kwa jina la Azzuri mjini Manaus  katika mchezo wa kundi D.

 
Italia walikuwa wa kwanza kuandika bao la kuongoza katika dakika ya 35 kupitia kwa Claudio Marchisio, lakini katika dakika ya 37,  Daniel Sturridge aliisawazishia England bao hilo akiunganisha krosi nzuri iliyochongwa na Wayne Rooney kutoka wingi ya kushoto.
 
`Supa` Mario Balotelli ndiye aliwaua England baada ya kuandika bao la pili kwa njia ya kichwa katika dakika ya 50.

Kikosi cha England kilichoanza:  Hart, Johnson, Cahill, Jaglielka, Baines, Gerrard, Henderson, Sterling, Rooney, Welbeck and Sturridge 
  
Kikosi cha Italia kilichoanza: Sirigu, Chiellini, Paletta, Barzagli, Darmian, De Rossi, Pirlo, Veratti, Candreva, Marchisio and Balotelli.





  • Edinson Cavan aliifungia Uruguay bao la kuongoza kwa njia ya mkwaju wa penati.
  • Joel Campbell, Oscar Duarte na Marcos Urena waliifungia  Costa Rica mabao yaliyowapa ushindi wa 3-1
  • Luis Suarez alikaa benchi, lakini hakutumika katika mchezo wa wa usiku huu.
  • - See more at: http://shaffihdauda.com/?p=2114#sthash.PwSsNkBz.dpuf


  • Edinson Cavan aliifungia Uruguay bao la kuongoza kwa njia ya mkwaju wa penati.
  • Joel Campbell, Oscar Duarte na Marcos Urena waliifungia  Costa Rica mabao yaliyowapa ushindi wa 3-1
  • Luis Suarez alikaa benchi, lakini hakutumika katika mchezo wa wa usiku huu.
  • - See more at: http://shaffihdauda.com/?p=2114#sthash.PwSsNkBz.dpuf
    KIKOSI cha Uruguay kimelala kwa bao 3-1 dhidi ya Costa Rica katika mechi ya kundi D kwenye Fainali za Kombe la Dunia 2014 zinazoendelea nchini Brazil. 

    Katika mechi hiyo, mshambuliaji mahiri wa Uruguay na Liverpool Luis Suarez alianzia benchi na kumalizia mechi benchi yaani hakucheza kabisa licha ya kuwepo kwenye orodha ya wachezaji wa akiba, na hii inatokana na kushindwa kuimarika ipasavyo kutoka kwenye majeruhi ya goti alilofanyiwa upasuaji.
     
    Wafungaji wa Costa Rica waliopeleka maumivu Uruguay ni Joel Campbell, Oscar Duarte na Marcos Urena. Uruguay walipata bao lao kwa mkwaju wa penalti kupitia kwa Edinson Cavani.

    0 comments:

    Post a Comment

    OFFICIAL MEMBER

    OFFICIAL MEMBER

    Please Share This Site

    HABARI ZETU

    LIKE PAGE YETU HAPA