Sunday 15 June 2014

Utabiri MPYA wa Nabii: Mwanamuziki mkubwa wa Bongo Fleva atafia Jukwaani kabla ya kumalizika kwa mwaka huu wa 2014




Nabii  anayetikisa  kwa  maono  ya  vitu  mbalimbali  Hosea  Chamungu  'Mzee  wa  maono'  ameibuka  na  jambo  zito  baada  ya  kufunga  kwa  siku  tatu  mfululizo  huku  akifanya  maombi  nyikani......

Akiongea  na  mwanahabari  wetu  mapema  wiki  hii, nabii  Chamungu  alisema  kuwa  amekuwa  na  desturi  ya  kufunga  siku  tatu  kila  wiki  ili  kupata  maono  ya  mambo  mbalimbali  yanayojiri  hapa  duniani.....

Chamungu  ambaye  kabla  ya  unabii  amewahi  kuwa  mwanachama  wa  Freemasons  amesema  alichofunuliwa  hivi  majuzi  ni  kwamba  bado  vifo  vitaendelea  kuwaandama  wasanii  mbalimbali  na  kabla  ya  kumalizika  kwa  mwaka  huu  wa  2014  kuna  msanii  mkubwa  wa  mziki  wa  Bongo  Fleva  atafia  jukwaani.....

"Atafariki  kwa  ajili  ya  pesa  na  itakuwa  jukwaani, yawezekana  akawa  anagombea  pesa  au  anatunzwa  pesa  jukwaani  ndipo  umauti  utakapomkuta,"  alisema  Chamungu  huku  akisisitiza  kuwa  hayo  ni  maono  na  si  hadithi.

Chamungu  alifafanua  kuwa  vifo  vinavyohusisha  pesa  hutokana  na  shetani  ambao  ni  jamii  ya  Lucifer  na  Illuminati  ambapo  pia  hujulikana  kama  Freemasons....

"Kifo  chake  kitavuta  hisia  za  watu  wengi  wakiwemo  wakawaida  na  maarufu  kama  ilivyotokea  kwa  marehemu  Kanumba  lakini  hatazikwa  na  watu  wengi  kama  alivyozikwa  Kanumba," alisema


0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA