Friday 11 July 2014

ANGALIA PICHA MAPOKEZI YA DIAMOND PLATNUMZ AKITOKEA MAREKANI KATIKA TUZO ZA BET


Tarehe 10/7/2014 ni siku ambayo Star wa muziki wa Bongo fleva nchini Tanzania Diamond Platnumz, ambaye anachafua anga la muziki kwa sasa kwa utunzi na uimbaji wake alitua katika Uwanja wa Ndege Mwal. Jurius Nyerere, mnamo mishare ya saa nne na nusu za usiku akitokea nchini Marekani ambapo alikua huko kushiriki katika Tuzo kubwa Dunia  BET awards, ambazo hufanyika kila mwaka, Diamond alikua katika kategori ya Best African Act ambayo ilichukuliwa na Davido kutoka Nigeria.
Watanzania wenye moyo wa Upendo na Kizalendo walijitokeza katika viwanja vya ndege kumpokea Msanii huyo, wakiwa na mabango makubwa kabisa yenye maneno ya kuashiria ushujaa aliouonyesha Diamond katika muziki na kuipeperusha vyema  Bendera ya Tanzania katika muziki, Uwanja wa ndege wa Mwl. Julius Nyerere, uligubikwa na Kelele za Furaha na Sauti zilisikika zikiimba wimbo wa Mdogomdogo ikiwa ni mapenzi ya dhati kabisa kwa Diamond kwa kutuwakilisha vema na kurejea salama, hakika kazi ya muziki wetu kwa sasa inaonekana.

Diamond baada ya kufika aliwashukuru wote waliofika kumpokea na kusema kuwa safari yake ilikua nzuri na amejifunza vitu vingi sana pia amekutana na watu wengi na tutaraji mengine mengi na mazuri katika muziki wetu, na kwa upande mwingine alitoa shukran za dhati kabisa kwa watanzania kuipokea vema video yake mpya ya mdogomdogo, imekua ikifanya vizuri sana na hata youtube imekuwa na views wengi kwa muda mchache




















 



na Matukio blog

0 comments:

Post a Comment

OFFICIAL MEMBER

OFFICIAL MEMBER

Please Share This Site

HABARI ZETU

LIKE PAGE YETU HAPA